Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 103 2022-11-08

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kituo kikubwa cha kupozea umeme Kwambwembwele Vibaoni?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Handeni, kwa niaba ya Mheshimwa Waziri wa Nishati, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanza kutekeleza mpango wa kuimarisha Gridi ya Taifa uliopewa jina ‘Gridi Imara’ kwa kujenga miundombinu ya usafirishaji na usambazaji umeme pamoja na vituo vya kupoza na kudhibiti umeme. Mpango huu una miradi zaidi ya 40 inayotekelezwa ndani ya miaka mitano kuanzia mwaka 2022/2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka 2022/2023 Serikali itajenga njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 132 kutoka Mkata kwenda Kilindi kupitia eneo la Kwambwembwele Vibaoni, Handeni Mjini. Katika mwaka wa fedha 2024/2025 kituo cha kupoza umeme kitajengwa na kupokea umeme kutoka katika njia ya Mkata/Kilindi itakayojengwa mwaka huu.