Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka ruzuku kwenye majiko madogo ya gesi?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwanza napongeze jitihada zinazoendelea kwa upande wa Serikali, lakini changamoto mojawapo inayofanya matumizi ya gesi kuwa yapo chini zaidi ni kukosekana kwa vituo vya kuuzia gesi, hasa katika maeneo ya vijijini ambayo yapo mbali na yanasabababisha kuongeza gharama kubwa kwenye mitungi pomoja na gesi kwa ujumla.

Je, Serikali ina mpango gani wa kurekebisha hali hiyo?

Jambo la pili, sambamba na gesi umezungumzia kuhusu kuwezesha nishati safi katika maeneo ya vijijini, bado maeneo ya vitongoji ambavyo ni vikubwa sana havijapata nishati safi ya umeme, Serikali ina mpango gani wa kuharakisha kufikisha nishati hiyo, sambamba na hii ya gesi. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Manyanya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali la kwanza, wakati wa utekelezaji wa huu mradi wa kutoa ruzuku, tunaamini wigo wa wafanyaji biashara kwenye eneo hili wataongeza na hivyo watafika katika maeneo yote kwa sababu Serikali itajitahidi kuhakikisha shughuli hii inapata ruzuku na hivyo wawekezaji mbalimbali wanaweza kushiriki. Pia, mwongozo tunaoutengeneza utaangalia namna ya kufanya, kama wanavofanya wenzetu wanaosambaza mbolea na maeneo kama hayo, ili tuweze kufika katika maeneo yote husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini, kwenye swali la pili la umeme wa vitongoji, Serikali inaendelea katika mzunguko wa tatu awamu ya pili ya REA, viitongoji baadhi vinapatiwa umeme, lakini pia kuna miradi ya jazilizi inaendelea katika maeneo yetu na Serikali inaendelea kutafuta fedha kuhakikisha kwamba vitongoji vyote vinapatiwa umeme ili wananchi waweze kutumia nishati hiyo safi.