Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 102 2022-11-08

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka ruzuku kwenye majiko madogo ya gesi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuweka mikakati ya kuhakikisha nchi inafikia zaidi ya asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2032. Miongoni mwa mikakati hiyo ni pamoja na kufanyika kwa mjadala wa Kitaifa wa nishati safi ya kupikia, kuunda kikundi kazi kwa ajili ya uratibu, kutenga fedha katika bajeti ya 2023/2024 kwa ajili ya shughuli za nishati safi ya kupikia, kuanzisha mfuko wa nishati safi ya kupikia pamoja na kuzitaka taasisi zote zenye watu zaidi ya 300 kama vile shule, vyombo vya ulinzi na usalama, Magereza na kadhalika, kutumia nishati mbadala kupikia ikiwemo gesi na kuachana na matumizi ya kuni na mkaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini inatarajia kutekeleza mradi wa majaribio kwa kutoa ruzuku ya asilimia 50 ya gharama zote (jiko, gesi, mtungi pamoja na vifaa vinavyohusiana). Katika Awamu hii vifaa vipatavyo 100,000 vitasambazwa katika Mikoa 25 ya Tanzania Bara. Naomba kuwasilisha.