Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha huduma za afya kwa Wazee badala ya kutumia Dirisha la Wazee ambalo linawatesa?

Supplementary Question 1

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pia nishukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa, mfumo huu wa kutumia dirisha la wazee unaonyesha una mapungufu makubwa. Je, Serikali haioni kuwa ipo haja sasa kubadilisha mfumo huu na ikiwezekana wazee wapewe kadi kabisa za bima ya afya, kuliko kupewa vitambulisho kama ilivyokuwa sasa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa wazee wengi wanaoishi vijijini hawajui kabisa kwamba kuna dirisha lile la afya, kutumia huduma za afya; je, Serikali ina mpango gani wa kuwafikia wazee hawa ili nao waweze kupata huduma hii muhimu kwao kama wazee wenzao wanaoishi mijini? (Makofi)

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninamshukuru sana Mheshimiwa Shabani Omari Shekilindi kwa maswali yake mawili ya nyongeza hususani katika kuhakikisha kwamba wazee wetu wanapata huduma bora za matibabu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba tubadilishe mfumo wa kutumia dirisha la wazee lakini tutumie mfumo wa bima ya afya kwa wote. Nitumie Bunge lako Tukufu kuwashawishi Waheshimiwa Wabunge wote, Ijumaa kupitisha Muswada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote, kwa sababu moja ya jambo ambalo linakwenda kutatua ni kuhakikisha kwamba wazee pia wanapata huduma za matibabu bila ya kikwazo cha fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Wizara ya Afya tunaamini kwamba, kutungwa kwa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote kutaboresha upatikanaji wa huduma za afya kwa wazee ikiwa ni pamoja na dawa. Kwa sababu wazee wengi sasa hivi wanakwenda kwenye dirisha la wazee, dawa hakuna, wakiwa na bima tunaamini watapata dawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Wazee wa Vijijini hawapati hii huduma, tumekinyanyua kile kitengo kilichokuwa kina shughulikia huduma za wazee, kimekuwa sasa ni section, kwa hiyo, kina Mkurugenzi Msaidizi, kazi yake kila siku ni kuangalia huduma za matibabu kwa wazee, huduma za rehabilitation pamoja na huduma za palliative za shupaa. Kwa hiyo, tunaamini kabisa pia hii itaongeza muamko katika kutatua changamoto za wazee. (Makofi)