Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 7 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 101 2022-11-08

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha huduma za afya kwa Wazee badala ya kutumia Dirisha la Wazee ambalo linawatesa?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimuwa Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuimarisha huduma za afya kwaa wazee. Kwa miaka mingi wazee wamekuwa wakipatiwa huduma mahsusi kwa kupitia madirisha maalum ya huduma za afya kwa wazee yaliyotengwa katika vituo vya kutolea huduma za afya. Katika kuimarisha huduma za afya kwa wazee, Wizara katika Mwaka huu wa fedha 2022/2023 imepitishiwa muundo mpya ambao umewezesha Wizara kuanzisha seksheni ndani ya Kurugenzi ya Tiba inayoshughulika na Huduma za Afya ya Wazee, Huduma za Utengamao na Huduma za Tiba Shufaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, chini ya Seksheni hii mpya, Utaratibu wa huduma mbalimbali za afya ya wazee utafanyika na maboresho ya huduma za afya kwa wazee yatapokelewa na kuchakatwa na kupatiwa majawabu kwa wakati. Rasimu ya mwongozo wa utekelezaji wa mkakati wa huduma za afya kwa wazee ipo katika ngazi ya maboresho hivi sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, uzee na kuzeeka havikwepeki, Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuwaenzi wazee wetu.