Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Haji Makame Mlenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. HAJI MAKAME MLENGE aliuliza: - Je, ni kwa nini wafanyabiashara wanaoweka bustani kando ya barabara hulipishwa fedha nyingi na TANROADS na TARURA?

Supplementary Question 1

MHE. HAJI MAKAME MLENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali hata hivyo na maswali mawili ya nyongeza.

Je, Wizara yako inayo mpango wowote wa kutengeneza bustani kando kando ya barabara hasa maeneo ya Mjini?

Swali la Pili, kwa kuwa mazingira ni muhimu. Je, Wizara yako inashirikiana vipi na Wizara ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira katika kuratibu mazingira, hasa bustani katika maeneo ya pembeni ya barabara? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Makame Mlenge Haji, Mbungwe wa Chwaka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria na Kanuni zimetoa maelekezo kwa watu wote ambao wanataka kutumia hifadhi ya barabara bila kuathiri matumizi wafike kwenye mamlaka husika ili waweze kuendeleza na kupendezesha Miji. Suala hili linafanyika kwa barabara za TANROADS, vilevile barabara za TARURA kwa maana ya TAMISEMI.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kuhusu kushirikiana na hifadhi ya mazingira ni kwamba taratibu na sheria inayoongoza iko chini ya Wizara ya Ujenzi. Kwa hiyo, tunahakikisha kwamba tukishampa mtu kazi, kwa maana ya kumpa kibali, basi anafanya kazi kulingana na miongozo na taratibu ambazo zimewekwa kwa mujibu wa Sheria na Kanuni ambayo inalinda kutumia hifadhi ya barabara. Ahsante.