Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 100 2022-11-08

Name

Haji Makame Mlenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. HAJI MAKAME MLENGE aliuliza: -

Je, ni kwa nini wafanyabiashara wanaoweka bustani kando ya barabara hulipishwa fedha nyingi na TANROADS na TARURA?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Makame Mlenge Haji, Mbunge wa Chwaka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Tozo kwa Wafanyabiashara wanaoweka bustani kando ya barabara hutozwa kulingana na Mwongozo wa Udhibiti wa Uwekaji Huduma ndani ya eneo la hifadhi ya barabara (Manual for Control of Utilities Installation within the Road Reserve) ambao unatokana na Kanuni ya 3 (1) ya Kanuni za Barabara (Fedha na Ushirikishwaji wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi) za mwaka 2011 zilizotolewa chini ya Sheria ya Barabara, Na.13 ya mwaka 2007. Kulingana na Mwongozo huo Wafanyabiashara wanaoweka Bustani kando ya barabara hutozwa Shilingi 4,639.5 kwa mita ya mraba kwa mwaka. Fedha hizo hupelekwa Bodi ya Mfuko wa Barabara kwa ajili ya kugharamia matengenezo ya barabara.