Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ya ujenzi wa Bwawa katika Mji wa Itolwa, Kata ya Jangalo itatekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante./ Kwanza kabisa nichukue nafasi hii kuishukuru sana Wizara ya Maji wamefanya kazi kubwa, lakini nina swali moja la nyongeza. Kijiji cha Ombiri kilikuwa na bwawa la asili ambalo sababu ya mvua kubwa kingo zake zimekatika. Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha wanarudisha bwawa lile kwa ajili ya watu wa kijiji kile? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Monni, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunafahamu bwawa la Ombiri katika Kijiji cha Ombiri, limepata matatizo, sisi kama Wizara kwa umuhimu wa bwawa namna ambavyo tunaendelea kuyajenga, kwa hiyo, bwawa hili ambalo limepata hitalafu sisi kama Wizara tumelipa kipaumbele, tutakuja kulitekeleza kwa kulikarabati vizuri.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ya ujenzi wa Bwawa katika Mji wa Itolwa, Kata ya Jangalo itatekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mradi wa Maji wa Nyantukuza, Jimbo la Nyangh’wale umeenda kukamilika na kwa sababu kuna ukame mkubwa wa maji, je, Serikali ina mpango gani wa kusambaza maji kutoka chanzo hicho kwenye kata zifuatazo: Nyidundu, Nyalubele, Shabaka, Kaboha na Mwingilo, je, Serikali ina mpango gani wa kusambaza maji hayo kwa haraka ili kupunguza adha hii ya ukame wa maji? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Nyangh’wale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli mradi ule ni mradi ambao tunatarajia uondoe matatizo ya maji katika kata hizo hizo ulizozitaja. Naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo sasa Wizara tunapambana kuona tunakabiliana na hili tatizo la ukame, tutafika na kuona uwezekano wa kuweza kusambaza maji katika kata alizozitaja Mbunge. Ahsante.