Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 7 Water and Irrigation Wizara ya Maji 98 2022-11-08

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: -

Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ya ujenzi wa Bwawa katika Mji wa Itolwa, Kata ya Jangalo itatekelezwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilikamilisha utafiti wa ujenzi wa bwawa la mita za ujazo 106,100 katika Kijiji cha Itolwa Wilayani Chemba. Gharama za ujenzi wa bwawa hilo ni shilingi bilioni 1.7 na katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa bwawa hilo. Maji yatakayohifadhiwa katika Bwawa la Itolwa yatatosheleza mahitaji ya wakazi wa Kijiji cha Itolwa.