Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Je, ni kwa kiasi gani Vyuo vya Serikali vimejiandaa kupokea wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza naishukuru Serikali kwa majibu mazuri yanayotia moyo. Hata hivyo majibu haya hajatoa takwimu; yaani hizi takwimu hazijaja na percent ili tuone ukubwa wa tatizo sisi kama wawakilishi wa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, mimi hapa nina takwimu ya chuo kimoja tu hiki cha MUHAS hapo Muhimbili. Mwaka 2022/2023 udahili, wanafunzi walioomba pale walikuwa 27,540; waliokidhi vigezo 19,287, lakini chuo kile kina uwezo wa kudahili wanafunzi 866 tu, ambayo ni 4% tu ya mahitaji: Je, hatuoni kwa trend hii kwamba tunakatisha tamaa vijana wetu kuendelea kusoma masomo ya Sayansi? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyowaelezakwenye majibu yangu ya msingi, tumeona ukubwa wa tatizo, ndiyo maana Serikali imeingia mkataba wa kuchukua mkopo huu. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari fedha hizi tumeshazipata na zinakwenda kutanua sasa wigo wa vijana wetu kuingia katika Masomo ya Sayansi. Amezungumzia suala la Muhimbili ambayo sana sana ni masomo ya tiba, lakini hapa tunazungumzia sayansi kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa takwimu zilizopo mwaka 2020 waliofanya mtihani wa kidato cha sita walikuwa ni 84,212; mwaka 2021 waliofanya mtihani wa form six walikuwa ni 88,273; na mwaka 2022 waliofanya mtihani wa form six walikuwa ni 94,456.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa takwimu hizi kama zaidi ya 40,000 wanakwenda kwenye masomo ya sayansi, yaani karibu asilimia 50 wanadahiliwa katika nyanja hiyo ya sayansi, bado tumesimama pazuri. Hata hivyo mradi huu unakwenda kutusogeza zaidi ya asilimia 70.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Je, ni kwa kiasi gani Vyuo vya Serikali vimejiandaa kupokea wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Hivi sasa wanafunzi wa vyuo vya afya nchini kwa ngazi ya cheti na diploma wanasoma kwa ghrama kubwa. Je, ni kwa nini sasa Serikali isione namna ya kuwapunguzia wanafunzi hawa gharama katika masomo yao ya fani ya afya kwa ngazi ya cheti na diploma ili wazazi waweze kumudu gharama zilizobaki?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Issaay, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tukiri kwamba ni kweli kwamba upande wa elimu ya tiba ada zimekuwa ni kubwa, lakini wakati tunatoa bajeti yetu hapa, wenzetu au benki yetu ya NMB ilitoa ufadhili wa zaidi ya shilingi bilioni 200 kwa ajili ya kada hizi za kati. Kwa hiyo, eneo la kwanza naomba wazazi na walezi wa wanafunzi hawa waweze kuifikia benki hii ili waweze kupata mikopo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Serikali tuko katika mpango mkakati wa kuhakikisha kwamba tunafikia kada hii ya kati pindi tutakapoongeza bajeti kwa ajili ya wanafunzi hawa kupata mikopo vilevile.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Je, ni kwa kiasi gani Vyuo vya Serikali vimejiandaa kupokea wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi?

Supplementary Question 3

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Katika Jimbo langu la Nachingwea kuna Chuo cha Ualimu lakini hakitoi kozi ya sayansi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha kozi ya sayansi katika chuo hiki cha Nachingwea?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Nachingwea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna Chuo cha Ualimu pale Nachingwea kwa vile Mheshimiwa Mbunge ametoa ushauri, naomba tuuchukue ushauri huu twende tukaufanyie tathmini ili tuweze kuangalia kama kuna uhitaji wa kuanzisha kozi hiyo ya sayansi katika chuo hicho.