Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 7 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 95 2022-11-08

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: -

Je, ni kwa kiasi gani Vyuo vya Serikali vimejiandaa kupokea wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatanyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Mradi wa Higher Education for Economic Transformation (HEET) inatarajia kuongeza fursa za wanafunzi wanaosoma masomo ya Sayansi katika Vyuo Vikuu na Taasisi za Elimu ya Juu kwa kujenga na kukaratabati miundombinu kama ifuatavyo: ujenzi wa maabara na karakana za kufundishia 108; vyumba vya mihadhara na madarasa 130; kumbi za mikutano ya kisayansi 23; mabweni 34; miundombinu ya shambani na vituo atamizi 10 kwa ajili ya kuendeleza ubunifu.

Mheshimiwa Naibu Spika, maboresho hayo yanatarajiwa kuongeza idadi ya wanafunzi wanaosoma programu za Sayansi kutoka wanafunzi 40,000 kwa mwaka 2020 hadi kufikia 106,000 mwaka 2026. Aidha, mradi huu pamoja na kuboresha mitaala zaidi ya 290 pia utasomesha wahadhiri 831 katika programu za kipaumbele.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile, kwa mwaka wa masomo 2022/2023, Serikali kupitia Samia Scholarship imetoa ufadhili wa asilimia 100 kwa wanafunzi 640 wenye ufaulu wa juu waliodahiliwa katika Vyuo Vikuu kusoma Programu za Sayansi, Teknolojia, Hisabati na Tiba.

Mheshimiwa Saibu Spika, nakushukuru sana.