Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Skimu ya Umwagiliaji ya Igurubi katika Jimbo la Igunga?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa skimu zilizojengwa katika Jimbo la Mhambwe, ikiwemo Nyendara, lumpungu, Kigina, Mgondogondo, Kahambwe, lili ziweze kuwasaidia wakulima wa jimbo hili?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika moja ya mikakati tuliyonayo katika mwaka huu wa fedha ni kuhakikisha tunakarabati na kukamilisha skimu ambazo tulizipitia na kuona zinahitaji marekebisho madogo ili wananchi waendelee kutumia kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba katika baadhi ya skimu katika Jimbo lake zitatekelezwa mwaka huu na nyingine katika mwaka ujao wa fedha. (Makofi)