Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA K.n.y. MHE. SALMA R. KIKWETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara ya Moka-Mtumbikile - Matimba kwa kiwango cha changarawe?

Supplementary Question 1

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, barabara hizi nyingi za Nyanda za Juu Kusini zimekuwa na changamoto ya mvua ya muda mrefu, na barabara nyingi hazijafikiwa kiwango cha changarawe. Ni upi mkakati wa Serikali? Na ukifuatilia maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuwa anazungumza na watu wa TARURA kwamba maeneo ya Kusini ambayo ni ya uzalishaji barabara hizo zijengwe kwa kiwango cha changarawe kwa wingi.

Je, ni upi mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba barabara hizi zinajengwa kwa kiwango cha changarawe, hususan kwenye Mikoa ya Ruvuma, Lindi na Njombe hususani Wilaya ya Makete?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sanga, Mbunge wa Jimbo la Makete kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali ni kwamba moja tunataka kuwahakikishia tunapandisha hadhi barabara za udongo kwenye changarawe na pili, zile za changarawe kuzipeleka katika kiwango cha lami; na tunafungua barabara nyingi mpya. Kwa hiyo sehemu ya miradi mikubwa ambayo tumeielekeza katika Nyanda za Juu Kusini ikiwemo Agri-connect ni ujenzi wa lami ili maeneo hayo yaweze kupitika muda wote na shughuli za kiuchumi ziweze kuendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Serikali ipo kazini na tutaendelea kuongeza fedha ili kuhakikisha hizi barabara ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja zinafanyiwa kazi.