Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 87 2022-11-08

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA K.n.y. MHE. SALMA R. KIKWETE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara ya Moka-Mtumbikile - Matimba kwa kiwango cha changarawe?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salma Rashid Kikwete Mbunge wa Jimbo la Mchinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) ilitenga Shilingi milioni 622.52 kwa ajili ya ujenzi wa vented drift yenye urefu wa Mita 45 na upana wa mita 7; ujenzi wa boksi kalavati kubwa katika mto Nangaru lenye urefu wa mita 26.8 na upana wa mita tisa; Kuchonga barabara yenye urefu wa kilomita 10.3, Kuweka changarawe kilomita mbili na kuchimba mifereji ya kuondoa maji barabarani.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia TARURA itajenga barabara ya Moka-Mtumbikile-Matimba kwa kiwango cha changarawe kadri ya upatikanaji wa fedha baada ya kukamilisha ujenzi wa vikwazo (Bottlenecks) vya barabara hiyo.