Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, ni nani mwenye jukumu la kusafisha mifereji na kuzibua makaravati ya barabara zinazojengwa chini ya TARURA au TANROADS?

Supplementary Question 1

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumuuliza Naibu Waziri kwamba kwa kuwa barabara nyingi zilizoko chini ya TARURA, mifereji yake imejaa takataka, imeota majani na ni nyingi na hasa zile Mjini. Na kwa kuwa, tunajua kwamba TARURA ina upungufu wa wafanyakazi: -

Je, Serikali haioni ni muhimu wakaishauri TARURA iingie mkataba agencies yoyote ambayo inaweza kusaidia kufanya usafi wa barabara hizi?(Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, wazo tumelipokea, lakini nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba zipo taratibu wa barabara hizi kufanyiwa usafi. Usafi ni pamoja na kufyeka, kuondoa mchanga, ama kuzibua makaravati yanayokuwa yameziba, kazi hizi huwa zinatangazwa ambapo Wakandarasi wanaomba na kupewa hizo Kandarasi kwa ajili ya kufanya huo usafi. Kwa hiyo utaratibu upo na barabara hizo zinasafishwa kwa upande wa TARURA TAMISEMI wanasimamia kuhakikisha kwamba barabara zinasafishwa lakini kwa barabara za TANROADS ambazo zipo chini ya Wizara ya Ujenzi pia zinasimamiwa kuhakikisha kwamba barabara hizi hazizibi kwa sababu ya uchafu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nitoe rai kwa watumiaji wa barabara kwamba sehemu kubwa ya kuziba hii barabara na uchafu wakati fulani ni kwa sababu ya kazi za kibinadamu ambazo watu wanafanya kazi kwenye hifadhi ya barabara na kusababisha tatizo hilo. Kwa hiyo, niwaombe wananchi kupitia nafasi hii kutokufanya kazi za maendeleo kwenye hifadhi za barabara kwa sababu zinazababisha barabara hizo kuziba. Ahsante. (Makofi)