Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Wodi ya Mama na Mtoto na chumba cha kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya Gidas?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. La kwanza: Kwa kuwa mahitaji ya wahudumu wa afya katika Kituo cha Afya Gidas ni 52 na waliopo sasa ni watano tu: Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza wahudumu wa afya ili kuwasaidia wananchi hawa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili: Kwa kuwa kituo cha afya kiko mbali na hospitali ya wilaya: Je, Serikali ipo tayari kupeleka gari la kubebea wagonjwa ili kuwasaidia wananchi wetu? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Daniel Baran Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na upungufu wa wahudumu wa afya, Serikali inatambua upungufu wa wahudumu wa afya katika maeneo mbalimbali ya vituo vyetu vya huduma na ndio maana wiki iliyopita, Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utumishi alitoa taarifa katika Bunge lako kwamba Serikali imeweka mpango wa kutoa vibali na kuanza kutoa ajira; na katika ajira hizo watumishi wa sekta ya afya watakuwemo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inafanya mkakati na mara watakapoajiriwa, tutahakikisha kituo hicho kinapata watumishi ili kuboresha huduma za afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na gari la wagonjwa, kama nilivyotangulia kujibu kwenye majibu ya msingi, magari ya wagonjwa 195 yatanunuliwa katika mwaka huu wa fedha na yatapelekwa kwenye Halmashauri zote ikiwepo Halmashauri ya Babati Vijijini. Kwa hiyo, kituo hicho pia kitapata gari la wagonjwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. (Makofi)

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Wodi ya Mama na Mtoto na chumba cha kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya Gidas?

Supplementary Question 2

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa Tabora Manispaa ina population kubwa ya watu zaidi ya 600,000; na pale Tabora Mjini kuna zahanati ambayo inazalisha watu 10 mpaka 20 kwa siku: Je, ni lini Serikali sasa itakuwa tayari ku-upgrade ile zahanati na kuwa kituo cha afya na kuiwekea wodi wa wazazi pamoja na theatre? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa
Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Munde, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inafanya tathmini ya maeneo ambayo yana zahanati, lakini yana idadi kubwa ya wananchi na yana umbali mkubwa kutoka kituo cha afya au hospitali. Tutafanya tathmini kwenye zahanati hii aliyoisema ili tuone kama inakidhi vigezo iweze kupandishwa hadhi kuwa kituo cha afya.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Wodi ya Mama na Mtoto na chumba cha kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya Gidas?

Supplementary Question 3

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Hospitali ya Mama na Mtoto, Chanika ina upungufu wa general wards za wanaume, wanawake na watoto ili kukifanya kituo cha afya kitoke kwenye hadhi ya kituo cha afya kuwa hospitali: Je, ni lini Serikali itajenga wodi hizi ili kuweza kuwasogezea huduma karibu wananchi wa Kata za Zingiziwa, Chanika, Mkuyuni, Kongola na Pugu? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry Silaa, Mbunge wa Jimbo la Ukonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Hospitali ya Mama na Mtoto ya Chanika ni hospitali ambayo inatoa huduma kwa akina mama lakini ina uhitaji wa wodi ya akina mama wajawazito na wodi ya watoto. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunafanya tathmini na pia tunatafuta fedha kwa ajili kwenda kujenga wodi katika hospitali ile ya Chanika ili sasa iweze kuwa na miundombinu yote kwa ajili ya kulaza akina mama na mtoto. (Makofi)

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Wodi ya Mama na Mtoto na chumba cha kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya Gidas?

Supplementary Question 4

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa fursa hii nami niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa sisi tuna vituo vya afya vya siku nyingi; Mkongo Gulioni, Mputa na Lusewa na havina vyumba vya upasuaji na wala Wodi ya Mama na Mtoto na vimechakaa sana: Je, Serikali inaweza kuwahakikishia wananchi wa Mkongo Gulioni, Mputa na Lusewa kama wapo katika list ya kukarabatiwa vituo vyao vya afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Natumbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tunatambua kwamba vituo hivi vya afya na vilivyo vingi nchini ni vya zamani ni vituo ambavyo vina upungufu wa miundombinu hususan majengo ya upasuaji na wodi. Ndiyo maana katika jibu la msingi nimesema, tunafanya tathmini kwenye vituo vya afya vyote ambavyo vina upungufu mkubwa wa miundombinu hasa majengo ya upasuaji na wodi ili baadaye tutafute fedha kwa ajili ya kuhakikisha majengo hayo yanajengwa. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika Jimbo la Namtumbo na vituo vya afya ambavyo amevitaja, tutavipa vipaumbele.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Wodi ya Mama na Mtoto na chumba cha kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya Gidas?

Supplementary Question 5

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nataka kujua, ni lini Serikali italeta fedha katika Kituo cha Afya cha Kisaki ambacho kimejengwa kwa nguvu za wananchi na Kituo cha afya cha Mwaja ambacho kilipokea shilingi milioni 250 za mwanzo?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mussa Sima, Mbunge wa Singida, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nawapongeza sana wananchi katika hicho kituo hicho cha afya ambao wamechangia nguvu zao na wanasubiri kuungwa mkono na Serikali. Niwahakikishie Serikali inatambua sana nguvu za wananchi na tutatafuta fedha, ikipatikana twende tukaunge mkono nguvu za wananchi kuhakikisha vituo vya afya vinakamilika. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Wodi ya Mama na Mtoto na chumba cha kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya Gidas?

Supplementary Question 6

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Hospitali ya Mji wa Tarime inakabiliwa na changamoto ya chumba cha kuhifadhi maiti kutokufanya kazi kwa takribani zaidi ya wiki tatu; na ukizingatia Hospitali ya Mji wa Tarime inahudumia zaidi ya Wilaya tatu, kwa maana hiyo, ina maana ina wagonjwa wengi, hivyo inakuwa na maiti nyingi ambazo zinahitajika kupelekwa Kituo cha Afya cha Sirari. Kwa sababu Halmashauri ya Mji wa Tarime haina fedha za kuweza kukarabati chumba kile cha kuhifadhi maiti, Serikali haiweze kuchukua jambo hili kwa udharura na kupeleka fedha ili kunusuru adha ambayo wanaipata Halmashauri ya Mji wa Tarime? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la jengo la kuhifadhia maiti kutofanya kazi katika Hospitali ya Mji wa Tarime, naomba nipokee taarifa hiyo na tutaifanyia kazi kwa haraka iwezekanavyo ili kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata huduma hiyo muhimu katika hospitali hiyo.