Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 32 2022-04-11

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Wodi ya Mama na Mtoto na chumba cha kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya Gidas?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Baran Sillo, Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali ilipeleka shilingi bilioni 1.04 kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Babati Vijijini kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri, Kituo cha Afya, Nyumba ya Mtumishi na ukamilishaji wa zahanati.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua uhitaji wa wodi ya mama na mtoto na chumba cha kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya Gidas.

Mheshimiwa Naibu Spika, kituo hiki kimeombewa fedha Hazina na ujenzi utaanza mara fedha zitakapotolewa.