Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Hopsitali ya Wilaya ya Pangani?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, bado Hospitali ya Wilaya ya Pangani inakabiliwa na changamoto ya uchakavu wa vifaa kama vile generator, mashine ya kufulia na ambulance: Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha inaondoa changamoto hiyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kupitia fedha za tozo, Kata ya Madanga tumepata shilingi milioni 500 kwa ajili ya kujenga Kituo cha Afya cha Kata ya Madanga: Je, ni upi mpango wa Serikali wa kuhakikisha inakwenda kukamilisha kituo hicho cha afya kwa haraka ili kuokoa maisha ya wananchi wa Kata ya Madanga, Kimang’a, Bushiri na Masaika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshemiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwantumu Mzamilu Zodo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Hospitali hii ya Pangani ni chakavu, sambamba na hilo, ina vifaa tiba na vifaa kama mashine za kufulia chakavu na pia gari la wagonjwa ni chakavu sana. Naomba kwanza nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Mwantumu Zodo kwa namna ambavyo anasemea wananchi wa Mkoa wa Tanga na Watanzania kwa ujumla, vile vile kwa namna ambavyo anashirikiana kwa karibu sana na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Pangani, Mheshimiwa Jumaa Aweso, ambaye naye pia amekuwa anafuatilia sana kuhusiana na ujenzi na ukarabati wa Hospitali ya Halmashauri ya Pangani.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mwaka huu wa fedha, Serikali imetenga fedha kwa ajili kununua magari 407 na kati ya hayo 195 ni magari ya wagonjwa na Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Pangani itapata gari jipya la wagonjwa na kuondoa changamoto hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la vifaa tiba Serikali imeendelea kutenga fedha na tutahakikisha tunaenda kwa awamu kuboresha vifaa tiba katika hospitali hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na kituo cha afya ambacho kimepata shilingi milioni 500, nimhakikishie kwamba kitakwenda kukamilishwa, kutafutiwa vifaa tiba na kuwekwa watumishi ili huduma za afya ziendelee kutolewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Hopsitali ya Wilaya ya Pangani?

Supplementary Question 2

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kama ilivyo kwa hospitali kongwe, tuna vituo vya afya vikongwe na chakavu sana kama Kituo cha Afya cha Gungu kilichopo Korogwe. Ni lini Serikali italeta mkakati wa ukarabati na kuboresha vituo vya afya vya siku nyingi na chakavu ili kuwapa huduma wananchi wetu? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshemiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mnzava Mbunge wa Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie kwamba Serikali imefanya tathmini ya vituo vya afya chakavu vyote nchini kote na mpango unandaliwa kuhakikisha vinakarabatiwa na vinakuwa bora kwa ajili ya utoaji wa huduma za afya. Kwa hiyo, kituo hicho pia kitapewa kipaumbele. Ahsante.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Hopsitali ya Wilaya ya Pangani?

Supplementary Question 3

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Magari ya vituo vya afya vya Mrijo, kwa Mtoro na Makorongo yamechakaa kabisa na hayafanyi kazi. Naomba commitment ya Serikali sasa kama tunaweza kufanyiwa ukarabati au kama tunaweza kupata magari mapya. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshemiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mohamed Monni, Mbunge wa Jimbo la Chemba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, nampongeza sana kwa kazi kubwa anayoifanya kwa wananchi wa Chemba. Nimhakikishie kwamba magari ya wagonjwa ambayo ni chakavu, Serikali inaweka mpango wa kutafuta magari mengine ya wagonjwa ili kuhakikishwa huduma za afya zinaenda vizuri na tutatoa kipaumbele katika vituo vya afya ambavyo Mheshimiwa Mbunge amevitaja. (Makofi)