Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je? Serikali ina mkakati gani wa kuzuia ukatali wa kijinsia na utumikishwaji wa watoto katika makambi yanayotarajiwa kujengwa ili kuwezesha ujenzi wa Bomba la Mafuta Hoima Tanga?

Supplementary Question 1

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi nami niulize maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na kwamba Mheshimiwa Waziri alisema kuna ngazi mbalimbali ambazo zinashughulika na hayo, lakini wanaonaje sasa wakati huu wasianzishe jeshi la jamii kama lilivyo Jeshi USU kwa upande wa Maliasili, kwa ajili ya kuhakikisha kwamba jamii inalinda watoto wetu dhidi ya ukatili pamoja na wanawake? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili: Ni kwa nini sasa Serikali isiende kwenye shule zetu kwa ajili ya kuanzisha klabu za stadi za maisha na majukwaa ya stadi za maisha kwa ajili ya kuwajengea watoto wetu uwezo wa kujilinda wenyewe? (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Nusrat kama ifuatavyo. Swali lake la kwanza kuhusu Jeshi Jamii; Wizara imejipanga na mpango kazi wa Taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWWA) ili kuhakikisha kwamba wanakuwa na usalama. Mpango huu umejielekeza kuanzia ngazi ya vijiji hadi mkoa na kuhusisha vyombo vya ulinzi na usalama katika kila eneo.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu jukwaa la watoto; Wizara yetu ina majukwaa ya watoto ambayo yanahimiza ulinzi na usalama. Pia yapo mabaraza na clubs za watoto kuanzia shule za msingi, sekondari hadi Vyuo. Klabu hizi zinawafunza watoto na kuwaelimisha waweze kujitambua, kujielewa, kujiamini na kujieleza wakati wowote katika kujikinga na ukatili dhidi ya watoto. (Makofi)

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je? Serikali ina mkakati gani wa kuzuia ukatali wa kijinsia na utumikishwaji wa watoto katika makambi yanayotarajiwa kujengwa ili kuwezesha ujenzi wa Bomba la Mafuta Hoima Tanga?

Supplementary Question 2

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mkoa wa Manyara umeonekana kuwa ni mbili mbili katika ukatili wa jinsia na sababu kubwa ni kwamba waathirika bado hawana elimu ya kutosha kuhusu hatua za kuchukua: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutokomeza ukatili wa jinsia katika Mkoa wa Manyara? Ahsante. (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

kuhusu swali la ukatili wa jinsia kwa watoto katika mkoa wako, Wizara kama nilivyoeleza imejipanga katika mpango wa Taifa kutokomeza ukatili wa jinsia (MTAKUWWA). Mpango huu unahusisha vijiji hadi mkoa.

Kwa hiyo, kuna Kamati katika kila mkoa ambazo zinahusisha usalama wa watoto na wanawake katika kuhakikisha tunatokomeza ukatili kwa watoto na tunapinga ukatili wa jinsia kwa wanawake na wananchi.