Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Je, Jiji la Arusha lina wamachinga wangapi, wapo maeneo gani na wangapi wamepatiwa vitambulisho hadi kufikia mwezi Februari, 2022?

Supplementary Question 1

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, kwanza taarifa iliyotolewa na Mheshimiwa Naibu Waziri nina mashaka nayo, kwa sababu wako wamachinga wengi Jiji la Arusha ambao wamekosa maeneo ya kufanyia baishara.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia taarifa ya Mheshimiwa Naibu Waziri ametuambia kwamba kwa sasa wao wamewatambua wamachinga 5,426 na kati ya hao wametoa vitambulisho kwa wamachinga 1187, je ni kwa nini wamachinga waliobaki mpaka sasa hivi hawajapata vitambulisho na wanaendelea kuchajiwa ushuru na Halmashauri ya Jiji la Arusha?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa mgambo ambao wanatumwa na Halmashauri ya Jiji la Arusha kupitia Mkurugenzi wa Jiji wamekuwa wanapora vitu vya watu vinakwenda kuwekwa kule depo vinaoza pia wanachukua fedha za watu nje ya utaratibu kiasi cha kuleta manyanyaso na kufanya hali ya kisiasa...

SPIKA: Mheshimiwa Gambo sasa hapo unachangia, Mheshimiwa Gambo ulishauliza maswali.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mrisho Mashaka Gambo Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba taarifa hizi zimetoka ndani ya Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa watendaji wa Serikali ambao wamejiridhisha idadi ya wamachinga walioko pale na idadi ya wamachinga ambao wamepewa vitambulisho. Pamoja na kwamba Serikali na Jiji la Arusha lilikuwa katika utaratibu wa kuwapanga wamachinga lakini utaratibuwa kutoa vitambulisho ulikuwa unaendelea sambamba na kuwapanga wamachinga; kwa hiyo nikutoe shaka katika eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na kwa nini baadhi ya hawa wamachinga hawajapata vitambulisho; suala hili ni suala la kutoa elimu, kuhamasisha wale wamachinga wenye sifa waweze kutoa kwa hiari yao ili waweze kupata vitambulisho vile na kazi hii inaendelea kuelimisha ili hawa waliobaki nao wapate vitambulisho.

Mheshimiwa Spika, kuhusu mgambo kuvamia na kupokea fedha na kumwaga bidhaa za wananchi, Serikali ilishatoa tamko, kwamba katika shughuli za kuwapanga wamachinga nchini kote mgambo hawahusiki na hawatakiwa kuhusika kuleta bugudha yoyote kwa wafanyabiashara. Kwa hiyo nitoe maelekezo kwa Jiji la Arusha kusimamia maelekezo ya Serikali ili wafanyabiashara hawa wasibughudhiwe na mgambo sehemu yoyote. Ahsante.