Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 21 2022-04-08

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: -

Je, Jiji la Arusha lina wamachinga wangapi, wapo maeneo gani na wangapi wamepatiwa vitambulisho hadi kufikia mwezi Februari, 2022?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mrisho Mashaka Gambo, Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hadi kufikia mwezi Februari, 2022 Jiji la Arusha lilikuwa na wamachinga 5,426 ambao walikuwa wamepangwa katika maeneo mbalimbali kama ifuatavyo; soko la Samunge, Kiwanja Na. 68 Soko la Kilombero, eneo la Ulezi Mianzini, Machame Luxuary na Kilombero eneo la Daladala.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuratibu usajili na utoaji vitambulisho vya wamachinga, ambapo kwa Halmashauri ya Jiji la Arusha jumla ya wamachinga 1,187 sawa na asilimia 22 wamepatiwa Vitambulisho.