Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali kukifanyia ukarabati Kituo cha Polisi cha Nansio?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwanza nitumie fursa hii kutoa pole kwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Ukerewe, kwa msiba wa askari uliopatikana jana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada hayo, nina maswali mawili ya nyongeza, la kwanza; kwa kuwa tathimini tayari imeshafanyika, lakini miundombinu iliyoko pale hasa mifumo ya maji safi na maji taka pamoja na mapaa ya kituo chenyewe na nyumba za watumishi ni mbovu sana, sasa Serikali haioni sababu kuchukua jambo hili kama la dharura na ikalifanyia kazi kwa haraka kadri inavyowezekana ili kujenga mazingira mazuri ya utendaji kwa watumishi wetu pale?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Mheshimiwa Waziri haoni sababu, namwomba ikiwezekana twende naye pale ili aangalie mazingira kwa uhalisia tuweze kujadiliana tuone namna njema ya kuboresha mazingira ya utendaji kwa watumishi wetu wa Ukerewe? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza alikuwa anaomba tuchukue jambo hili kama dharura; basi kwa sababu Mheshimiwa Mbunge anakifahamu vizuri kituo hiki naomba nikubaliane naye kwamba tunalichukulia hili jambo kama la dharura. Kwa hiyo nitatoa maelekezo kufuatilia, kuona jinsi gani ambavyo tunaweza tukafanya ili yale mambo ya dharura tuweze kuyafanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kuhusu suala la mimi kwenda kwenye Jimbo lake, hilo halina tatizo, tutapanga ratiba baada ya Bunge hili kumalizika ili tuweze kwenda kutembelea jimbo lake kuona wenyewe jinsi ambavyo tunaweza kusaidiana kutatua changamoto za kidharura ambazo Mheshimiwa Mbunge amezieleza.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali kukifanyia ukarabati Kituo cha Polisi cha Nansio?

Supplementary Question 2

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kumekuwa na ukosefu wa amani katika baadhi ya maeneo hasa katika Kata ya Ngaya na kata ya Buriye na kupelekea wananchi sasa kuweza ku-share na Mbunge wao ambaye ni mimi kujenga Kituo cha Polisi na sasa kimefikia kwenye hatua ya lenta. Sasa swali langu ni lini Mheshimiwa Waziri atafika kuja kuweka jiwe la msingi sambamba na kutenga fedha kuja kumalizia Kituo hicho cha Polisi? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi, Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na wananchi wake kujitolea kujenga kituo hiki na kama ambavyo nilivyokuwa nimejibu jana kwa zile jitihada ambazo zimeanzishwa na wananchi, tumeshajitahidi kuziendeleza. Tuna mfuko wetu wa tozo na tozo, japokuwa hauwezi kukidhi maeneo yote, lakini tutajitahidi kuangalia tutakachoweza kufanya ili tuongeze jitihada hizo ambazo Mheshimiwa Mbunge na wananchi wake wamezifikia. Nitakuwa tayari kwenda kuweka jiwe la msingi wakati wowote ambapo Mheshimiwa Mbunge mimi na yeye tutashauriana yaani muda muafaka wa kuweza kufanya kazi hiyo.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali kukifanyia ukarabati Kituo cha Polisi cha Nansio?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona, kwa miaka 20 sasa Wilaya ya Kilolo haina Makao Makuu ya Polisi na wala kwenye Wilaya penyewe hakuna Kituo cha Polisi.

Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi za viongozi mbalimbali kujenga Makao Makuu ya Polisi katika Wilaya ya Kilolo kwenye Mji wa Kilolo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri kwamba Mheshimiwa kwenye Jimbo lake la Kilolo kama ambavyo Wilaya kadhaa zimekuwa zina ukosefu wa Vituo vya Polisi vya Wilaya na hii ni moja kati ya mambo ambayo jana niliyazungumza na mikakati ya Kiserikali ya kiujumla ya kukabiliana na tatizo hili, hivyo nimwombe Mheshimiwa Mbunge avute Subira, lakini suala hili tumelichukua kwa uzito wake.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali kukifanyia ukarabati Kituo cha Polisi cha Nansio?

Supplementary Question 4

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza msitu wa Rubya umetoa milioni 50 kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi, pale Rubya.

Je, Serikali ipo tayari kuwaongezea fedha ili kituo hicho kiweze kukamilika pamoja na nyumba za maaskari?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli fedha hizo zimetolewa, lakini mpaka sasa taarifa nilizokuwa nazo ni kwamba kazi hizi zinaendelea vizuri na hakujaonekana dalili za kushindwa kukamilika wala wafadhili hawajaonesha dalili ya kushindwa kuendelea kukamilisha kituo hiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba tuwape muda wakamilishe tuone watafikia wapi, kama kutatokea changamoto baadaye, basi tutaangalia namna gani ya kuweza kulikabili.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali kukifanyia ukarabati Kituo cha Polisi cha Nansio?

Supplementary Question 5

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kituo cha Polisi cha Wilaya Bunda ni chakavu sana na Mheshimiwa Waziri anakijua, amefika pale na kinahudumia Majimbo matatu Mwibara, Bunda Mjini na Bunda. Je, ni lini Mheshimiwa Wizara atakikarabati kituo hicho ili kiendane na hadhi ya Wilaya?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Kituo cha Bunda kiko chakavu na binafsi nakumbuka niliwahi kutembelea kituo hiki na hata Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo hili naye vilevile alinikumbushia juu ya ukubwa wa changamoto hii. Hivyo basi, nimhakikishie Mheshimiwa Ester Bulaya kwamba tunafahamu na pale ambapo hali ya kibajeti itakapokaa vizuri, basi tutakifanyia kazi kituo hiki.

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali kukifanyia ukarabati Kituo cha Polisi cha Nansio?

Supplementary Question 6

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kata ya Kilungule, Jimbo la Mbagala wananchi wamejenga Kituo cha Polisi kwa nguvu zao, lakini sasa ni mwaka wa tatu Serikali haijafanya juhudi ya kufungua kituo hicho. Je, ni lini Wizara italeta watumishi ili kituo hicho kifanye kazi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Janejelly, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kituo hiki vilevile nakifahamu nakumbuka wakati ambapo tunaanza jitihada za kujenga hiki tulishiriki kufanya harambee. Niwapongeze sana wananchi walioshiriki lakini niwahakikishie kwamba juhudi hizo za wananchi hazitapotea bure kwa vituo vyote ambavyo wananchi wametoa nguvu zao, basi Serikali tutaangalia kadri itakavyowezekana, hali itakaporuhusu tuweze kuvikamilisha.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali kukifanyia ukarabati Kituo cha Polisi cha Nansio?

Supplementary Question 7

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Napenda kuuliza kwamba,je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kituo cha Polisi Nanyamba kwa sababu sasa hivi Nanyamba ni Makao Makuu ya Halmashauri ya Mji wa Nanyamba na kuna changamoto za kiulinzi kule mpakani? Nakushukuru.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chikota, Mbunge wa Nanyamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna mpango wa kujenga vituo vikubwa zaidi, kukarabati, kujenga vipya katika maeneo ambayo hakuna, lakini mambo haya hatuwezi kuyakamilisha kwa wakati mmoja na ndio maana hata ukiangalia bajeti inayokuja mwaka huu tunatarajia kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Makao Makuu ya Polisi Mtwara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mnaona jitihada ya Serikali tunaenda hatua kwa hatua. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kuwa hata Makao Makuu ya Mtwara tunataka kujenga, ina maana hata changamoto za Wilaya nazo tutazifanyia kazi hatua kwa hatua. Kwa hiyo nimwombe mvute Subira.