Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 16 2022-04-06

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: -

Je, nini mkakati wa Serikali kukifanyia ukarabati Kituo cha Polisi cha Nansio?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uchakavu wa Kituo cha Polisi Nansio kilichopo Ukerewe. Tathmini kwa ajili ya ukarabati imeshafanyika mwaka huu wa 2022 na kubaini kuwa kiasi cha shilingi 68,000,000 zinahitajika ili kugharamia ubadilishaji paa, dari, mfumo wa maji na maji taka, pamoja na kuziba nyufa, kurekebisha sakafu pamoja na kupaka rangi. Ukarabati huu utafanyika kulingana na upatikanaji wa fedha.