Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuchimba mabwawa ya kuhifadhia maji kwa ajili ya kunyweshea mifugo katika kila Kijiji nchini?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu haya ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shilingi bilioni mbili aliyoisema kwenye majibu yake ya msingi, ni ndogo sana kutokana na swali lilivyoulizwa wa kila Kijiji kuchimbwa mabwawa.

Je, Serikali ina mpango gani sasa kuongeza bajeti ili maeneo haya anayoyasema yaweze kuchimbwa mabwawa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; tumeleta maombi ya Mbulu Vijijini kuchimbiwa mabwana katika vijiji vya Gidihim, Eshkesh, Yaeda, Masieda na Endagichan na wewe Naibu Waziri unafahamu: Lini mtatuchimbia hayo mabwawa kama tulivyoomba?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Flatei Massay. La kwanza ni juu ya kuongezwa kwa bajeti. Nimelipokea jambo hili na kwa kuwa sasa ndo tuko kwenye Bunge la Bajeti, namwomba Mheshimiwa Flatei Massay na Waheshimiwa Wabunge wengine, tusiwahishe shughuli; tusubiri, nina imani mambo mazuri yanakuja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni hivi vijiji vyake alivyovitaja. Naomba mimi na yeye tuzungumze mara baada ya hapa kuona namna ambavyo tunaweza kujipanga kwa ajili ya kutekeleza kile alichokiomba. Ahsante. (Makofi)

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuchimba mabwawa ya kuhifadhia maji kwa ajili ya kunyweshea mifugo katika kila Kijiji nchini?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi hii. Serikali iliwaahidi wananchi wa Kijiji cha Kivingo Kata ya Lunguza ambao wako pembezoni mwa hifadhi ya Taifa Mkomazi, kuwajengea bwawa kwa ajili ya shughuli za kilimo na lambo kwa ajili ya shughuli za ufugaji; na Mamlaka ya Hifadhi Tanzania (TANAPA) ilikuwa imeanza huo mchakato. Sasa ni lini Serikali itahakikisha kwamba bwawa hili linachimbwa na lambo kwa ajili ya mifugo linapatikana?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali zuri la Mheshimiwa Rashid Shangazi, Mbunge wa Mlalo juu ya ahadi iliyotolewa na Shirika letu la TANAPA kuhusu kujenga lambo katika Kijiji cha Kizingo pembeni ya hifadhi ya Taifa ya Mkomazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Serikali tunafanya kazi kwa pamoja na TANAPA ni chombo chetu, naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge ya kwamba nitazungumza na Mheshimiwa Waziri wa Maliasiri na Utalii tuwakumbushe TANAPA tuweze kuifanya kazi hii ya wananchi. Ahsante.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuchimba mabwawa ya kuhifadhia maji kwa ajili ya kunyweshea mifugo katika kila Kijiji nchini?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Naishukuru Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Miezi michache iliyopita Waziri wake alifika kwenye Jimbo langu akaangalia hatari kubwa ya lambo la Salamakati ambalo bado kidogo sana kutoweka. Kutokana na mvua zilizonyesha, lambo lile lina hatari kubwa sana ya kubomoka lote. Mheshimiwa Waziri aliahidi kuweka mikakati ya dharura ya kuziba lile lambo kabla halijabomoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kupata majibu kuna mikakati gani ya kuziba lambo la Salama ambalo liko hatarini kubomoka?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Naibu Waziri anaweza kunieleza nini kuhusu namna gani anaweza kwenda kuziba hilo lambo au kulijenga upya au kuliziba ile nyufa inayotaka kubomoka?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza tumepokea shukrani kutoka kwa Mheshimiwa Boniphace Getere. Pili ni juu ya ukarabati wa hili lambo. Naomba nilichukue jambo hili na kwenda kulisukuma ili liweze kufanyika sawa na ahadi ya Mheshimiwa Waziri.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuchimba mabwawa ya kuhifadhia maji kwa ajili ya kunyweshea mifugo katika kila Kijiji nchini?

Supplementary Question 4

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Bwawa la Mtera lililoko Halmashauri ya Iringa Vijijini kumekuwa na upungufu mkubwa wa Samaki na hivyo kuathiri biashara ya samaki katika Nyanda za Juu Kusini na masoko mengine.

Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kujenga mashamba darasa ya samaki hasa Jimbo la Kalenga ili sasa tuweze kufundisha vijana wengi kufuga samaki na hivyo kufufua uchumi wa vijana kwa namna hiyo? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, juu ya mashamba darasa ya kufugia samaki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo program ambayo itakwenda katika baadhi ya Halmashauri zetu na yawezekana kabisa moja ya Halmashauri itakayofaidika na program hii ya mashamba darasa ya samaki ikawa ni Halmashauri ya Kalenga.

Kwa hiyo, naomba nilichukue jambo hili la Mheshimiwa Mbunge ili tuweze kulifanyia kazi na wananchi wa Kalenga waweze kufaidika. (Makofi)

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuchimba mabwawa ya kuhifadhia maji kwa ajili ya kunyweshea mifugo katika kila Kijiji nchini?

Supplementary Question 5

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi. Serikali iliahidi Bwawa la Mhanga katika Halmashauri ya Itigi na wakaanza ujenzi, lakini ukasimama: Je, Waziri yuko tayari kwenda nami kuona utekelezaji wa ahadi hii nzuri ya Serikali ili wananchi wawaone aweze kusukuma malizio lile lambo ambalo linajengwa pale Muhanga?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishe kaka yangu Mheshimiwa Massare, niko tayari kwenda Itigi. (Makofi)