Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 2 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 14 2022-04-06

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuchimba mabwawa ya kuhifadhia maji kwa ajili ya kunyweshea mifugo katika kila Kijiji nchini?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Regina Ndege Qwaray, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha maeneo yenye mifugo mingi na yale yaliyoathirika na ukame mara kwa mara yanakuwa na miundombinu ya maji yakiwemo mabwawa kwa ajili ya maji ya mifugo. Katika kutekeleza mkakati huo, mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga shilingi bilioni 2.146 kwa ajili ya uchimbaji na ujenzi wa mabwawa au malambo na visima virefu vya maji kwa ajili ya mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha za kuchimba, kujenga na kukarabati mabwawa ama malambo na visima virefu kulingana na upatikanaji wa fedha. Aidha, napenda kutoa wito kwa Halmashauri za Wilaya, wafugaji na wadau wengine kuchimba na kujenga malambo au mabwawa, visima virefu kwa ajili ya maji ya mifugo. Pia, nahimiza wafugaji kuwa na vyanzo vyao binafsi vya maji kwa ajili ya mifugo yao.