Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Stendi ya Madaba ikizingatiwa kwamba stendi hiyo ipo kwenye eneo la kimkakati?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninaishukuru Serikali kwa majibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, imepita miaka minne tangu Serikali Kuu ilipobaini kwamba andiko la mradi wa Stendi ya Madaba halikukidhi vigezo. Ni hatua gani za haraka ambazo Serikali Kuu ilizichukua wakati huo ili kuhakikisha kwamba stendi hii inajengwa na inawanufaisha wananchi wa Madaba ili kuongeza mapato kwa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kama upembuzi yakinifu unakusudiwa kufanywa kwenye bajeti ya mwaka 2022/2023, ni lini sasa kwa uhakika stendi ya Madaba itajengwa? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NABU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Joseph Kizito Mhagama, Mbunge wa Jimbo la Madaba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge aliuliza tu kwamba andiko la awali ambalo limechukua takribani miaka minne na alichotaka kufahamu ni hatua gani ambazo Serikali ilizichukua baada ya hili andiko kukataliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi ambacho tulikifanya kwa kutumia wataalam wetu tulilirudisha lile andiko katika Halmashauri ya Madaba na baada ya kufanya hivyo waliainishiwa maeneo ya kufanya marekebisho. Kwa hiyo, jukumu la kuandika andiko ni la Halmashauri ya Madaba na ndio maana hata sasa hivi tumewarejea tena ili waandike upya haraka iwezekanavyo ili sisi tutafute fedha hii stendi iweze kukamilika. Kwa hiyo, mara watakapokuwa wamekamilisha kwa wakati basi na sisi tutatafuta fedha ili tuweze kujenga stendi hiyo kwa manufaa ya wananchi wa Madaba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu upembuzi yakinifu mara utakapokamilika ameuliza lini, ni kwamba watakavyomaliza andiko na mimi naamini tutajiridhisha kwamba kama andiko linakidhi vigezo likishakamilishwa mara baada tutakapopata fedha tutaanza mara moja kuhakikisha mradi ule unaanza. Ahsante. (Makofi)

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Stendi ya Madaba ikizingatiwa kwamba stendi hiyo ipo kwenye eneo la kimkakati?

Supplementary Question 2

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa fursa hii ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuiuliza Serikali ni lini itaisaidia Wilaya ya Ngara kuweza kujenga stendi mpya na ya kisasa? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NABU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Ndaisaba George, Mbunge wa Ngara kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, anachotaka kujua tu ni lini tutawasaidia kujenga stendi mpya na naamini kwamba moja ya miradi ya kimkakati katika Halmashauri nyingi ni pamoja na kuwa na stendi mpya. Kwa hiyo, kama Halmashauri yake itakuwa imewasilisha andiko maana yake kazi kubwa ambayo tunaifanya sasa ni kutafuta fedha, mara tutakapopata fedha maana yake ujenzi huo na wenyewe utaanza. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Stendi ya Madaba ikizingatiwa kwamba stendi hiyo ipo kwenye eneo la kimkakati?

Supplementary Question 3

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kufahamu hivi karibuni Makamu wa Rais alivyokuwa pale Bukoba Mjini aliwasilisha ahadi ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, kwamba Bukoba Mjini sasa tutajengewa stendi kuu ya mabasi. Kwa hiyo, ninataka kufahamu ni lini hiyo ahadi itatekelezwa na Bukoba tutapata stendi kuu ya mabasi ili kufungua Mkoa wetuwa Kagera na nchi za jirani? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NABU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Neema Lugangira Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kikubwa ambacho Wabunge wote wanapaswa kufahamu wakiwemo Mheshimiwa Neema Lugangira ni kwamba ahadi zote za Viongozi zipo katika hatua ya utekelezaji. Kikubwa tumeshaziainisha, tumeshazipa vipaumbele, jukumu letu sasa hivi ni kutafuta fedha kuhakikisha hizo ahadi zinatekelezeka.

Kwa hiyo, pesa itakapokuwa imepatikana hii ahadi ya Makamu wa Rais na yenyewe itatekelezeka kama ambavyo ameahidi. Kikubwa ni kwamba ahadi zote za viongozi zitatekelezwa. Ahsante. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Stendi ya Madaba ikizingatiwa kwamba stendi hiyo ipo kwenye eneo la kimkakati?

Supplementary Question 4

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Liwale ilikuwa na mradi wa kimkakati wa stendi lakini fedha zililetwa zikarejeshwa baada kukwama kwenye manunuzi.

Je, fedha zile zitarejeshwa lini ili mradi ule uendelee?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NABU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Jimbo la Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla hatujabadilisha sheria na ninyi mnakumbuka mwaka jana, fedha zote ambazo zilikuwa zinavuka mwaka zilikuwa zinarejeshwa Hazina, maana yake mnatakiwa kuanza kuomba upya.

Kwa hiyo, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba nimesikia maombi hapa ambayo ameyainisha na tutakwenda pale Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili kuona namna bora ya kusaidia kwa zile fedha ambazo awali zilikuwa zimeshapelekwa. Ahsante sana. (Makofi)