Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 11 2022-04-06

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Stendi ya Madaba ikizingatiwa kwamba stendi hiyo ipo kwenye eneo la kimkakati?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Joseph Kizito Mhagama, Mbunge wa Jimbo la Madaba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba kuwa na stendi ya mabasi katika Mji wa Madaba ili kuboresha upatikanaji wa huduma na kuongeza mapato ya Halmashauri hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Madaba katika mwaka wa fedha 2018/2019 iliandaa na kuwasilisha Serikali Kuu andiko la Mradi wa Kimkakati kwa ajili ya ujenzi wa stendi ya mabasi ambalo halikukidhi vigezo. Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba imepanga kutumia Shilingi Milioni Tano, kwa ajili ya kukamilisha upembuzi yakinifu (feasibility study) kwa ajili maandalizi ya andiko la mradi wa ujenzi wa stendi litakalowasilishwa Serikali Kuu ili iweze kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo wa kimkakati.