Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miradi ya umwagiliaji katika Tarafa ya Malangali ili wananchi waweze kushiriki katika kilimo cha umwagiliaji?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Spika, wananchi wa Tarafa ya Malangali hususan Kata za Nyololo, Maduma, Ihoanza, Idunda mpaka Mbalamaziwa wanafuatilia kwa umakini sana pengine kufahamu commitment ya Serikali, ni lini sasa kwa maana kama ni mwezi au kama ni mwaka wa fedha watapata matumaini ya kupata huu mradi wa umwagiliaji kutokana na changamoto kubwa sana ya ukame kwenye maeneo yao?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kilimo cha umwagiliaji na Serikali pia inatambua kwamba eneo la Mufindi ni kati ya maeneo ambayo kuna wakulima wengi na uzalishaji wake utaongeza tija kwenye kilimo cha nchi yetu ya Tanzania. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti inayokuja kwa maana kuanzia mwezi Julai tutatenga fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba uhakiki huo unakamilika, tukisha-establish mahitaji baada ya hapo sasa tutakwenda kwenye hatua inayofuata ambayo itakuwa ni hatua ya ujenzi kutokana na mahitaji.

Mheshimiwa Spika, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge na kwamba zoezi hilo litaanza mapema mwezi wa Saba ambapo uhakiki huu utafanyika na baadaye tutaenda katika hatua ya ku-establish mahitaji.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miradi ya umwagiliaji katika Tarafa ya Malangali ili wananchi waweze kushiriki katika kilimo cha umwagiliaji?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Bwawa la umwagiliaji la Edayaya Tlawi katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu ilifanyiwa usanifu toka 2009; je, ni lini sasa Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa bwawa hilo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Issaay, Mbunge wa Mbulu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja kati ya mikakati ambayo tumeiweka hivi sasa kama Wizara, tumeiagiza Tume ya Umwagiliaji wa Taifa ku-take stock ya miradi yote ya umwagiliaji katika nchi yetu ya Tanzania ile ambayo ilishafanyiwa upembuzi yakinifu ambayo ilishafanyiwa usanifu na baadaye kinachofanyika ni kwamba tutakwenda katika mradi mmoja baada ya mwingine iko miradi ambayo inahitaji fedha kidogo na iko miradi ambayo inahitaji fedha nyingi.

Mheshimiwa Spika, kupitia maelekezo haya ambayo Mheshimiwa Waziri ameyatoa, Tume hivi sasa wameanza zoezi hilo. Tutaipitia miradi yote na hivi sasa tunayo miradi 51 ambayo imeshatangazwa kupatikana kwa wakandarasi, naamini kupitia utaratibu huu ambao tumeuanzisha, tutaifikia miradi yote ikiwemo mradi ambao Mheshimiwa Mbunge ameusema.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miradi ya umwagiliaji katika Tarafa ya Malangali ili wananchi waweze kushiriki katika kilimo cha umwagiliaji?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa katika Manispaa ya Iringa katika Kata ya Isakalilo kuna Mradi wa Mkoga katika Kata ya Kituli kuna Mradi wa Kitwilu. Hii miradi ni ya muda mrefu sana. Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kutoa pesa ili wananchi hasa akinamama na vijana waweze kujiajiri kupitia hii miradi kwa kulima mbogamboga na matunda?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum wa Mkoa wa Iringa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika majibu yangu ya awali kwamba miradi yote hii na hasa katika Mkoa wa Iringa tumeshatenga fedha tayari kwa ajili ya Tume yetu kukamilisha kazi hii ya uhakiki. Bahati nzuri Mheshimiwa Rais ametuongezea bajeti kutoka shilingi bilioni 17 mpaka bilioni 51, nataka nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba katika kuelekea ajenda 1030 ya kukuza kilimo katika nchi yetu, moja ya kipaumbele ni kilimo cha umwagiliaji, hivyo hatutaacha mradi wowote nyuma, miradi yote tutajenga tukipata fedha ambazo zitatuwezesha kufikia malengo hayo.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miradi ya umwagiliaji katika Tarafa ya Malangali ili wananchi waweze kushiriki katika kilimo cha umwagiliaji?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi hii. Naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri; je, mifereji iliyo kwenye Kata ya Kilema na Kirua Vunjo na ile skimu ya Kahe wanaifahamu? Mbona haijawahi kuangaliwa siku za karibuni? Ahsante sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Charles Kimei, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, miradi yote ya umwagiliaji nchini inafahamika na ndiyo maana katika maelezo yangu ya awali nilisema tunayo miradi mingi sana. Tumeielekeza Tume badala ya kuendelea kukumbatia miradi mingi ambayo haifanyi kazi, tunaanza ku-take stock kupata mradi ambao unahitaji marekebisho madogo, mradi ambao unahitaji marekebisho makubwa, baadaye tuweke nguvu kukamilisha miradi hii ikiwemo mradi wa Mheshimiwa Mbunge.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miradi ya umwagiliaji katika Tarafa ya Malangali ili wananchi waweze kushiriki katika kilimo cha umwagiliaji?

Supplementary Question 5

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza. Kuna bwawa kubwa pale Kijiji cha Nyamgogwa, Kata ya Shabaka tumeshafanya upembuzi yakinifu na tumeshapeleka andiko mezani kwa Mheshimiwa Waziri, tunahitaji milioni 500 kwa ajili ya kulifufua ama kuliandaa bwawa hilo ambalo linanufaisha zaidi ya vijiji 20. Je, Waziri anatoa majibu gani kuhusu andiko letu hilo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hussein Amar, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge andiko lake kweli lipo mezani na hivi sasa kwa sababu ya ufinyu wa bajeti tumekuja na mfumo mwingine ambao pia umesaidia ujenzi wa skimu hizi ambao tunakwenda kuutambulisha mfumo huu. Nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba na yeye pia tutamuingiza kwenye mfumo huo ambao tumeufanya na tumeanza kuufanya kwa Mheshimiwa Mtaturu pale katika miradi ya Magonyi.

Mheshimiwa Spika, mfumo huu tutamchukua benki, tutamchukua na off taker wa mazao ya wakulima na kwa pamoja tunamwomba benki arekebishe miundombinu ya eneo lile, halafu mazao yatakayolimwa katika eneo lile tutamtafuta muuzaji ili basi itumike gharama hiyo ya benki kurekebisha. Wakati huo huo wauzaji wapate uhakika wa mazao yao ya kilimo na mwisho wa siku tutakuwa tumetatua changamoto ya ukosefu wa masoko ya wakulima wetu, lakini pia mradi huu utakuwa umekamilika. Mfumo huu unaitwa Tripartite Agreement ndiyo ambao tunaenda kuutekeleza katika miradi mingi ya skimu za umwagiliaji. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miradi ya umwagiliaji katika Tarafa ya Malangali ili wananchi waweze kushiriki katika kilimo cha umwagiliaji?

Supplementary Question 6

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa sababu miradi mingi ambayo Serikali inaiongelea ni ile ambayo ilijengwa miaka ya zamani na teknolojia ambayo imekuwa ikitumika ni ile ambayo ni ya mifereji ambayo inatumia maji mengi sana na inaharibu maji unnecessary. Kuna teknolojia mpya ambayo inatumika na tunaona katika nchi za jirani. Je, Serikali iko tayari kwenda kutumia teknolojia mpya ambayo inatumia maji kidogo lakini inakuwa na ufanisi zaidi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Kandege, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama Serikali tupo tayari kuendelea kutumia teknolojia ambayo italeta ufanisi katika kilimo cha umwagiliaji na hivyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, bahati nzuri Mheshimiwa Waziri na mimi mnatuona pale ni vijana ambao pia ni wa kidigitali, kwa hiyo tutahakikisha ya kwamba tunapitia kuona mifumo mbalimbali hasa yenye kuleta ufanisi ambayo naamini kabisa kama ni mfumo ambao Mheshimiwa Mbunge ameuzungumza hapa ambao utaleta tija kwa wakulima wetu sisi tuko tayari kuutumia mfumo huu na tutaelekeza pia Tume ya Umwagiliaji kuhakikisha kwamba inafanya utafiti wa kugundua teknolojia mbalimbali ili kumletea tija mkulima wetu wa Tanzania. (Makofi)

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miradi ya umwagiliaji katika Tarafa ya Malangali ili wananchi waweze kushiriki katika kilimo cha umwagiliaji?

Supplementary Question 7

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza. Kwa kuwa wananchi wa Tarafa ya Gonja katika Wilaya ya Same kwa takriban miaka kumi sasa wameomba kujengewa Bwawa la Yongoma ili lisaidie umwagiliaji katika Kata kame za Ndungu na Maore na design ilishafanywa na wajapan tangu 2012. Je, ni lini Serikali itajenga bwawa hili? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kaboyoka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika bajeti inayokuja mwaka 2022/2023 tumetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa 19, natumai pia na bwawa la Mheshimiwa litakuwemo ndani ya ujenzi huo. (Makofi)