Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 1 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 5 2022-04-05

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga miradi ya umwagiliaji katika Tarafa ya Malangali ili wananchi waweze kushiriki katika kilimo cha umwagiliaji?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile, Mbunge wa Mufindi Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Iringa unakadiriwa kuwa na eneo linalofaa kwa kilimo la hekta 54,000. Kati ya hizo hekta 20,017 zinamwagiliwa ambapo hekta 16,789 zinamwagiliwa kipindi cha masika na hekta 3,550 zinamwagiliwa kipindi cha kiangazi.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji inaendelea na uhakiki wa maeneo yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji katika Wilaya ya Mufindi ambapo hadi sasa skimu nne (4) zenye jumla ya hekta 1,800 zimehakikiwa na kuwekwa kwenye mpango wa umwagiliaji. Aidha, Tume inaendelea na uhakiki wa maeneo mengine yanayofaa kwa umwagiliaji ikiwemo Tarafa ya Malangali.

Mheshimiwa Spika, zoezi la uhakiki litakapokamilika, Tume ya Umwagiliaji itaandaa mpango kazi utakaoainisha kazi zitakazofanyika katika skimu hizo.