Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawavuna tumbili katika Kisiwa cha Juma Wilayani Sengerema ambao wanakula mazao ya wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Spika, pamoja na Serikali kuwa tayari kuhamisha makundi hayo ya tumbili hao katika Kisiwa cha Juma, lakini bado kuna tatizo la mamba katika mialo yetu hasa mwalo wa Buyagu, Irunda pamoja na Rugongo.

Je, Serikali ipo tayari kutujengea vizimba kwa ajili ya kuondoa huo usumbufu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili ni kwamba tunalo eneo katika Wilaya ya Sengerema kule kwa mwenzangu Ndugu yangu Eric Shigongo tunaeneo la Kichangani ambalo linatumika kwa ajili ya uvuvi. Jimbo la Sengerema linapata samaki kutoka katika eneo hilo.

Je, Serikali iko tayari kutuachia lile eneo likaondoka katika game reserve kwa sababu linatoa usumbufu watu walioko pale wanalipa kama wako nchi nyingine?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tabasam Hamis Mwagao Mbunge wa Sengerema kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kumekuwa na tatizo la mamba na si sehemu ya Sengerema peke yake, ni maeneo mengi ambayo yana mito na maziwa na Serikali imeendelea kujenga vizimba vya mfano. Lakini tunaelekeza pia Serikali za Mitaa tushirikiane nao ili kuhakikisha maeneo haya tunayaimarisha vizuri na wananchi waweze kupata huduma bora ya maji na pia tutashirikiana na Wizara ya Maji ili kuona kwamba wananchi wanaweza kupata maeneo mazuri ya kuchota maji badala ya kutumia maeneo ambayo yanawanyama wakali na waharibifu hususani mamba.

Mheshimiwa Spika, swali lingine ameongelea kuhusu eneo la Kichangani; eneo hilo liko katikati ya pori ambapo ni hifadhi na tuliweza kuwaruhusu wavuvi waweze kulitumia kwa utaratibu maalum kwa sababu tunatunza mazalia ya samaki na uhifadhi mbalimbali, hivyo nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge na wananchi kwamba eneo hili liko purposely kwa ajili ya uhifadhi.