Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 10 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 156 2022-11-11

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawavuna tumbili katika Kisiwa cha Juma Wilayani Sengerema ambao wanakula mazao ya wananchi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Tabasam Hamis Mwagao, Mbunge wa Jimbo la Sengerema kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya kazi ya kuyabaini na kuyadhibiti makundi (familia) ya tumbili yanayosumbua wananchi katika Kisiwa cha Juma, Wilayani Sengerema. Aidha, Serikali itaendelea kuhamisha makundi hayo na kuyapeleka katika hifadhi nyingine zenye mahitaji ya wanyamapori hao. Wizara itaendelea kuimarisha doria za kudhibiti wanyamapori waharibifu wakiwemo tumbili na nyani.