Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je, kuna mkakati gani kuiwezesha GST kufanya utafiti wa kisayansi na teknolojia kuhusu Critical Minerals ili kudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa?

Supplementary Question 1

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu ya Serikali kuhusiana na utayari wao kwenye suala la madini muhimu.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tumeona thamani ya fedha kwenye ongezeko la asilimia 9.4 kwenye bajeti ya GST mwaka wa fedha huu unaoendelea ambapo mapato yame-shoot mpaka asilimia 141.
Ni kwa nini sasa Serikali isilete mkakati wa dharura kwa ajili ya ku-fund GST ili iweze kufanya tafiti za kisayansi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili; sasa hivi tunapozungumza GST imefikia wapi na Serikali imefikia wapi kwenye masuala ya critical minerals kwenye utafiti na uchimbaji? (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Nusrat Hanje, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la kwanza; ili kuboresha teknolojia ya kutafuta madini na hasa tafiti ya madini haya ya kisasa, GST kupitia Wizara yetu ya Madini imeanza mkakati rasmi wa kuanzisha mashirikiano na wadau mbalimbali wa ndani na nje na kuandika maandiko mahsusi ambayo yatatusaidia kupata fedha za kuwekeza katika utafiti wa madini ya kimkakati. Tuna Kampuni ya Noble Helium ambayo inashirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na GST, tuna Kampuni ya Rocket Tanzania Limited.

Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la pili kuhusu hatua ambazo tumeshafikia katika kutafiti na kuzalisha madini ya kimkakati; ni kwamba sisi kupitia Tume yetu ya Madini kama Wizara, tayari tunatoa leseni za utafiti wa madini ya kimkakati kwa ajili ya utafutaji wa madini na uchimbaji wa madini. Na Serikali imekuwa na ubia na baadhi ya kampuni hizo na kwa ruhusa yako naomba nitaje chache.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Mkoa wa Lindi, tuna kampuni inayoitwa Lindi Jumbo Limited wenye leseni ya uchimbaji wa kati na wanaendelea na utafiti na sasa hivi wamefikia hatua ya kuendeleza ujenzi wa eneo la mradi.

Mheshimiwa Spika, hapo hapo Mkoani Lindi tuna Kampuni inaitwa Ngwena Tanzania Limited, wana leseni za utafiti wa madini ya kinywe na sasa hivi wako katika hatua ya uthamini kwa ajili ya ulipaji wa fidia. Na pia wale wa Jumbo nao wanafanya utafiti wa madini ya kinywe.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa hizi chache nipende tu kumhakikishia kwamba sasa hivi Tanzania imeamka na wawekezaji wakubwa wa ndani na nje wanajihusisha na utafutaji wa madini ya kimkakati. Ahsante sana.