Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 10 Energy and Minerals Wizara ya Madini 152 2022-11-11

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani kuiwezesha GST kufanya utafiti wa kisayansi na teknolojia kuhusu Critical Minerals ili kudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nusrat, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Madini imeielekeza Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kuandaa taarifa kuhusiana na madini mkakati (Strategic/Critical Minerals) hasa madini teknolojia ikiwemo madini muhimu kwa ajili ya nishati ya kijani (green energy minerals). GST imeanza kuandaa andiko kuhusiana na madini haya na kuainisha ni madini yapi ndiyo ya kimkakati kwa mtizamo wa dunia na nchi, matumizi ya madini hayo na mahala yanapopatikana.

Aidha, GST imebaini maeneo ya kufanya tafiti za jiofizikia katika maeneo sita (blocks) kwa nishati ya kijani (green energy) na matumizi ya magari ya umeme. Serikali inaendelea kutafuta wadau wa maendeleo ambao watashirikiana katika kufanya tafiti za jiosayansi. Ahsante sana.