Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, nini hatma ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Geita – Nyarugusu hadi Kahama hususani kipande cha Geita – Nyarugusu – Bulyanhulu?

Supplementary Question 1

MHE TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya swali hili ambayo yanaonekana yanatia moyo kwamba kuna majadiliano. Lakini niiombe Serikali majadiliano hayo yasichukue muda mrefu sana. Pamoja na majibu haya mazuri na swali moja la nyongeza.

Katika kuchochea uchumi shirikishi na shindani kuna barabara ndani ya Jimbo la Busanda kutoka Katoro kupita Kaseme kwenda Ushirombo, Jimboni Bukombe; je ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara hiyo ambayo imeishafanyiwa upembuzi yakinifu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Tumaini Magessa, Mbunge wa Busanda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Katoro hadi Ushirombo imeishafanyiwa usanifu na sehemu ya barabara hii inatekelezwa na Mpango ama Mradi wa RAIS, lakini sehemu iliyobaki itaendelea kuhudumiwa na TANROADS na Serikali ina mpango wa kutafuta fedha kukamilisha barabara yote kipande kitakachobaki baada ya kile kipande kitakachojengwa na Mpango wa RAIS kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, nini hatma ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Geita – Nyarugusu hadi Kahama hususani kipande cha Geita – Nyarugusu – Bulyanhulu?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, barabara ya kutoka Mkomazi – Mnazi - Umba junction Maramba hadi Tanga iko katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ukrasa wa 177 kwamba ijengwe kwa kiwango cha lami; je, ni lini sasa mchakato wa kuanza upembuzi yakinifu utaanza katika barabara hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shangazi, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja inayounganisha Mkoa wa Tanga na Mkoa wa Kilimanjaro iko kwenye Ilani na utekelezaji wa Ilani unaendelea. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tunahakika kwamba tutaanza usanifu wa kina baada ya kufanya upembuzi katika kipindi hiki cha miaka mitano katika utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi, ahsante.

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, nini hatma ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Geita – Nyarugusu hadi Kahama hususani kipande cha Geita – Nyarugusu – Bulyanhulu?

Supplementary Question 3

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Spika, nakushuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, Serikali iliahidi kuwajengea Wananchi wa Jimbo la Nkenge Wilaya ya Misenyi barabara ya Mtukura kwenda Minziro na nikupongeze Mheshimiwa Naibu Waziri na wewe ulifika na barabara hiyo sasa imeamza kujengwa, lakini ahadi ilikuwa ni ujenzi wa kiwango cha lami; je ni lini sasa barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kyombo, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ilikuwa inafunguliwa na tumeishaifungua na baada ya kuifungua hatua inayofuata nikufanya upembuzi na usanifu na ndiyo tunavyoelekezwa na ilani kwamba barabara zote ziwe kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge hiyo barabara itafanyiwa upembuzi na usanifu wa kina kadri fedha itakavyokuwa inapatikana, ahsante.

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, nini hatma ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Geita – Nyarugusu hadi Kahama hususani kipande cha Geita – Nyarugusu – Bulyanhulu?

Supplementary Question 4

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, ahsante, kuhusu ujenzi wa barabara ya Morogoro - Njombe boarder Serikali imedhamiria kujenga kilometa 100 kwa maana ya lot one na lot two.

Swali naomba Serikali ithibitishie Wananchi wa Mrimba je, ni lini hizi kilometa 100 kwa lot zote hizi mbili zitaanza kujengwa? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kunambi, Mbunge wa Mlimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunavyosema sasa hivi zabuni zimeishaandaliwa na tuko kwenye hatua za mwisho kutangaza hizo lot mbili ambayo ndiyo barabara inayokwenda kuunganisha na barabara ya Kibena - Madeke, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, nini hatma ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Geita – Nyarugusu hadi Kahama hususani kipande cha Geita – Nyarugusu – Bulyanhulu?

Supplementary Question 5

MHE. ASK. JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Kwa kuwa Mheshimiwa Rais alipofika Bunju B, aliahidi kwamba barabara ya Bunju B kupitia Mabwepande itajengwa kwa kiwango cha lami; je, unaweza kuwahakikishia wananchi wa Mabwepande kwamba itawekwa kwenye bajeti ijayo 2022/2023?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Gwajima, Mbunge wa Kawe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, bahati nzuri na mimi nimeitembelea hii barabara na kama alivyoomba iwepo kwenye bajeti Bunge hili ndiyo litaamua hiyo barabara ipitishwe kuwa kwenye bajeti, lakini sisi kama Wizara tunategemea kuipendekeza iwepo kwenye mpango wa kujengwa kwa kiwango cha lami kwa kuwa pia ni ahadi ya Mheshimiwa Rais, ahsante.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, nini hatma ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Geita – Nyarugusu hadi Kahama hususani kipande cha Geita – Nyarugusu – Bulyanhulu?

Supplementary Question 6

MHE. AGNESS E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, ahsante; ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami kipande cha barabara kutoka Masasi kwenda Nachingwea?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hokororo, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Masasi - Nachingwea kilometa 45 imepangiwa bajeti kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami, lakini pia kipande cha Masasi - Nachingwea hadi Liwale pia kimeingizwa kwenye Mpango wa EPC+F ambapo wakandarasi tayari wameishaoneshwa barabara hiyo na tayari tunategemea pengine kufungua zabuni kipindi si kirefu, ahsante.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, nini hatma ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Geita – Nyarugusu hadi Kahama hususani kipande cha Geita – Nyarugusu – Bulyanhulu?

Supplementary Question 7

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Spika nakushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na mpango wa Serikali wa kujenga barabara ya bypass kuanzia Kata ya Kisaki - Unyamikumbi - Unyambwa mpaka Mtipa na feasibility study imeshafanyika; nataka kujua tu commitment ya Serikali ni lini ujenzi huu utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema usanifu umeishakamilika, sasa hivi Serikali inatafuta fedha ili tuweze kuanza kujenga kipande hicho cha bypass, ahsante.