Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 10 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 147 2022-11-11

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: -

Je, nini hatma ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Geita – Nyarugusu hadi Kahama hususani kipande cha Geita – Nyarugusu – Bulyanhulu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tumaini Bryceson Magessa, Mbunge wa Busanda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika makubaliano ya msingi ya awali kati ya Serikali na Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Barrick, Kampuni ya Barrick ilikubali kutoa dola za Kimarekani milioni 40 kugharamia ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami. Hivyo, Serikali na Kampuni ya Barrick zimekubaliana kuwa fedha hizo kiasi cha dola za Kimarekani milioni 40 zitumike kwa ujenzi wa barabara ya Kahama – Bulyanhulu junction – Geita yenye kilometa 120 na kipande cha Bulyanhulu junction hadi Kakola (kilometa 11.3). Kwa sasa Serikali iko katika hatua ya kukamilisha majadiliano hayo ili kuwezesha mradi huo kuanza kutekelezwa, ahsante.