Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA aliuliza: - Je, ni lini Mahakama ya Wilaya ya Korogwe itajengwa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA: Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri, lakini kwa sasa hivi hatuna Mahakama ya Wilaya na shughuli za Mahakama ya Wilaya zinafanyika kwenye Mahakama yetu mojawapo ya Mwanzo ambayo haikidhi mahitaji ya Mahakama ya Wilaya: Huoni kuna haja sasa ya Serikali kuharakisha ujenzi wa Mahakama yetu ya Wilaya ya Korogwe? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza shughuli za Mahakama ya Wilaya ambazo zilitakiwa zifanywe na Mahakama ya Wilaya katika Wilaya ya Korogwe, mwanzo zilikuwa zinafanyika katika ofisi ndogo sana ya Mkuu wa Wilaya ya Korogwe. Kwa sasa tumeweza kukarabati jengo ambalo tumepewa na Halmashauri ya Korogwe ambalo kimsingi linakidhi mahitaji ya Mahakama hiyo. Hivyo basi, kama tulivyokwishatoa maelezo ya msingi kwenye jibu la msingi kwamba, ifikapo kipindi kijacho cha fedha, tunakwenda kuanzisha ujenzi wa Mahakama ambayo sasa itakuwa ni ya Wilaya ya Korogwe. Ahsante.