Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 83 2022-11-07

Name

Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA aliuliza: -

Je, ni lini Mahakama ya Wilaya ya Korogwe itajengwa?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Alfred James Kimea, Mbunge wa Korogwe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mahakama ya Tanzania inaendelea kutekeleza mpango wake wa miaka mitano wa Ujenzi na ukarabati wa majengo ya Mahakama katika ngazi mbalimbali. Kutokana na mpango huo wa Mahakama, jengo la Mahakama ya Wilaya ya Korogwe, limepangwa kujengwa katika mwaka wa fedha 2023/2024.

Mheshimiwa Spika, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa, Mahakama ya Tanzania ipo katika mpango wake wa ujenzi na ukarabati wa Mahakama zake hapa nchini. Hivyo basi, ujenzi wa Mahakama za Makao Makuu ya Tarafa zote nchini utakamilika ifikapo 2025.