Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza programu ya kuunda na kurusha setilaiti?

Supplementary Question 1

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali. Nina swali dogo la nyongeza kwamba nchi ya Uganda, siku ya jana tarehe 6 imekuwa ni nchi ya 12 katika Afrika kurusha Setilaiti yake angani. Setilaiti ile imeundwa kwa kupitia vijana ma- engineer wa Uganda wakishirikiana na nchi ya Japan na Kituo cha Anga cha Marekani: Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha program hii ya kuanza kufundisha vijana wetu kwa kushirikiana kama ilivyofanyika Uganda ili tuweze kupata setilaiti ambayo itaundwa na Watanzania halisi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kenneth Ernest Nollo, Mbunge wa Bahi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nchi za Afrika mpaka sasa tuna setilaiti 41 na kuanzia mwaka 2016 ni setilaiti takribani 20 ambazo tayari zimekuwa angani. Katika hizo setilaiti 41 ni tisa tu ambazo zimekuwa designed, manufactured na baadaye kupelekwa angani ambazo zina asili ya Kiafrika.

Mheshimiwa Spika, bado tuna maeneo mengi ya kuendelea kujifunza, lakini kama nilivyojibu katika swali la msingi, Mheshimiwa Rais siku ya tarehe 8 Februari wakati akiwa na kikao kazi na Wakuu wa Mikoa, alielekeza Wizara yetu ili tuone umuhimu sasa wa kuwa na setilaiti yetu. Tayari Wizara yetu imeshaunda timu ya wataalam ambao watakuja kuishauri Serikali aina ya setilaiti itakayoendana na mahitaji ya Watanzania. Ahsante.