Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kuwasikiliza na kufanyia kazi hoja za wamachinga, hasa baada ya zoezi la kuwapanga?

Supplementary Question 1

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Je, kuna katazo lolote la watu hawa (wamachinga) kupangwa katika maeneo ya wazi katika halmashauri na maeneo ya taasisi?

Pili; je, Serikali inaweza kutoa ruhusa kwa ajili ya wamachinga, hasa waliokuwa wanauza mananasi, kuweza kujipanga eneo la Railway na wale wa samaki kurudi eneo la Manyema? (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Priscus Jacob Tarimo, Mbunge wa Moshi Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inawajali sana wananchi wake, hasa wafanyabiashara wadogowadogo. Rais ametoa shilingi milioni 10 kwa kila mkoa kwa ajili ya kujengwa ofisi za wafanyabiashara wadogowadogo.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tayari imeshachora michoro hiyo kwa ajili ya ujenzi huo. Wafanyabiashara hawaruhusiwi kufanya biashara zao katika maeneo ya wazi na ya taasisi. Wafuate maelekezo ya viongozi wao wafanye biashara katika maeneo waliyopangiwa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili, eneo la wazi la Manyema, Moshi limetengwa kwa ajili ya shughuli za reli. Wafanyabiashara hawaruhusiwi kufanya biashara kwa ajili ya usalama wao, lakini pia kuzuia shughuli za shirika la reli hiyo.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Moshi tayari imeshawatengea wafanyabiashara hao walioondoshwa katika eneo la Reli la Manyema kufanya biashara zao katika maeneo mengine. Ahsante. (Makofi)