Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Community Development, Gender and Children Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum 74 2022-11-07

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: -

Je, nini mpango wa Serikali kuwasikiliza na kufanyia kazi hoja za wamachinga, hasa baada ya zoezi la kuwapanga?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Priscus Jacob Tarimo, Mbunge wa Moshi Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inafanyia kazi hoja za wamachinga, hasa baada ya zoezi la kuwapanga kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ambapo Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya hukukutana nao mara kwa mara kwenye vikao na kujadiliana nao kupitia viongozi wao kwa lengo la kushughulikia hoja na kero zao.

Mheshimiwa Spika, katika ngazi ya Taifa, Serikali inasikiliza hoja zao kupitia viongozi wa Shirikisho la Umoja wa Machinga (SHIUMA) Taifa. Kutokana na vikao vinavyofanyika, Serikali imeweza kuwajengea uwezo katika masuala ya uongozi na utatuzi wa changamoto zao. Pia watendaji wa kata sehemu mbalimbali nchini ikiwemo kwenye masoko wamekuwa na mchango mkubwa katika kuwasikiliza na kufanyia kazi hoja na kero zao kwa kadri zinavyojitokeza. Ahsante.