Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Makambako wataongezewa posho kama ilivyo katika Halmashauri nyingine nchini?

Supplementary Question 1

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nina maswali mawili ya nyongeza, pamoja na majibu mazuri ya Serikali swali lina maelezo madogo.

Kwa kuwa, fedha nyingi zinapelekwa za maendeleo katika Halmashauri zetu nchini zikiwepo za afya, barabara, maji, elimu. Na kwa kuwa hivi karibuni Rais wetu mpendwa mama Samia Suluhu Hassan ametupatia fedha nyingi za kujenga madarasa katika sekondari zetu Mabilioni kwa Mabilioni. Sasa Madiwani hawa hawasimamii kwenye force account hawamo, na hawa ndiyo wanaowaeleza wananchi tumepata fedha kiasi gani.

Je, Serikali haioni sasa ni muda muafaka Madiwani hawa wawemo ili kusudi maana ndiyo wanaowaambia wananchi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa vilevile kama nilivyosema ndiyo wanaosimamia na Serikali posho za mwezi tulizungumza kwenye bajeti hapa tunaomba waongezewe. Je, Madiwani wote nchini, bajeti ya 2023/2024 Serikali imejipangaje kuwaongezea posho za mwezi madiwani hawa nchini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Jimbo la Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba hospitali ya Awamu ya Sita, chini ya Mheshimiwa Rais, Samia Suluhu Hassan imeleta fedha nyingi sana katika Halmashauri zetu katika utekelezaji wa miradi mbalimbali. Lakini nimhakikishie kwamba kwa mfumo wa force account, kwa kuwa Waheshimiwa Madiwani ni viongozi wasimamizi wa miradi hiyo, mwongozo wa haukuwaweka Madiwani kuwa sehemu ya Kamati zile kwa sababu wanahitaji kuhoji zile Kamati. Kwa hiyo, kama Diwani atakuwa sehemu ya Kamati ile atashindwa kujihoji mwenyewe lakini atashindwa kusimamia wananchi katika maeneo yale katika kutekeleza miradi ile.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ninamuombe Mheshimiwa Mbunge aamini kwamba dhamira ya Serikali ni nzuri kwamba Waheshimiwa Madiwani wabaki na nguvu zao za kusimamia na kuhoji Kamati ili miradi iweze kutekelezwa kwa ubora zaidi.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na posho za Waheshimiwa Madiwani, kwanza niwahakikishie kwamba Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan anathamini na anajali sana kazi kubwa inayofanywa na Waheshimiwa Madiwani na ndiyo maana katika mwaka huu wa fedha amechukua jukumu la Serikali Kuu kulipa posho za Madiwani kama Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie kwamba Serikali inafanya tathmini ya kuona uwezekano na uwezo wa Serikali kuongeza posho hizo ili muda ukifika posho hizo ziongezeke kwa ajili ya Waheshimiwa Madiwani. Ahsante. (Makofi)