Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 69 2022-11-07

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: -

Je, ni lini Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Makambako wataongezewa posho kama ilivyo katika Halmashauri nyingine nchini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga Mbunge wa Jimbo la Makambako kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikiwalipa Madiwani wa Mamlaka za Serikali za Mitaa ikiwemo Halmashauri ya Mji Makambako posho kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Mitaa Sura 287 na 288 na kwa kuzingatia Kanuni za Kudumu za Halmashauri husika.

Mheshimiwa Spika, kuanzia mwaka 2019 Halmashauri ya Mji Makambako imekuwa ikilipa posho ya vikao ya Shilingi 50,000 ikiwa ni Shilingi 10,000 zaidi ya kiwango kilichopendekezwa. Aidha, hivi sasa viwango vya posho za safari kwa Halmashauri hiyo vinalipwa kwa kuzingatia waraka wa zamani kwa sababu viwango vya posho mpya havikutengewa bajeti ya mwaka 2022/2023, kwa kuwa wakati maelekezo ya mabadiliko ya posho hizo yanatoka tayari Bajeti ya Halmashauri ilikuwa imeandaliwa na kupitishwa kwenye vikao vya Kisheria vya Maamuzi.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Mji wa Makambako inashauriwa kufanya mapitio ya bajeti au izingatie maelekezo ya Waraka Na. 1 wa Utumishi wa Umma wenye Kumb. Na. CAC.17/228/01/A/176 wa Tarehe 10 Juni, 2022 kwenye bajeti ya mwaka ujao wa fedha.