Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. MOHAMED JUMAH SOUD aliuliza: - Je, Kampeni ya AFR 100 imetekelezwa kwa kiasi gani na maendeleo gani yamefikiwa hadi sasa?

Supplementary Question 1

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa nchi yetu Tanzania hivi sasa inakabiliwa na wimbi kubwa la ukataji na uchomaji moto wa misitu ya asili. Je, Wizara ina mkakati gani wa ufuatiliaji kuona mpango huu wa AFR 100 unakwenda kufanikiwa ili kukabiliana na tatizo la uharibifu wa misitu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa utekelezaji wa lengo la mpango huu linajumuisha nchi nzima pamoja na Zanzibar. Naomba tu kujua tumeishirikishaje Zanzibar ili kuona mpango huu tunautekeleza kinchi zaidi ili kuweza kukabiliana na tatizo la uharibu wa misitu kule Zanzibar? Ahsante sana.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Soud Mohammed Jummah, Mbunge wa Donge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa mhifadhi mzuri kwenye masuala haya ya misitu kwa sababu kwa asilimia kubwa amekuwa anatoa mchango mzuri sana kwenye eneo hili la uhifadhi.

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mikakati mingi na mikakati hii tayari ilishaanza kutekelezwa tangu mwaka 2018 ambapo Serikali iliingia mkataba na dunia. Mkakati huu ni wa kidunia lakini kwa Afrika tumeelekezwa kutekeleza jumla ya hekta milioni 100 kuziongoa ili ziingie kwenye uhifadhi. Tanzania ni moja ya nchi ambazo zimeingizwa katika mkakati huo ambapo jumla ya hekta milioni 5.2 tumeziwekea mkakati huo na malengo yetu ni kuhakikisha tunaziongoa.

Mheshimiwa Spika, mikakati hii imeendana sambamba na zoezi la uongoaji na urejeshaji wa maeneo ya hifadhi. Hivi karibuni utashuhudia ziara ya Mawaziri Nane wamekuwa wakitembea kila mikoa kuhakikisha kwamba maeneo yale ambayo yanastahili kurejeshwa, yarejeshwe ili tuweze kuingia kwenye mpango huu wa kidunia ambao tunaongoa jumla ya hekta milioni 350.

Mheshimiwa Spika, swali lake lingine ambalo ameuliza, je, Zanzibar ni miongoni mwa nchi ambazo ziko ndani ya mkakati huu. Zanzibar ni kweli ipo na kwa kuwa Zanzibar ni sehemu ya Muungano zoezi hili linafanyika kama Tanzania Bara na Zanzibar hivi karibuni kuna Mradi wa FAO ambao umeunganisha Zanzibar na Kigoma na tayari wanatekeleza katika maeneo mbalimbali ikiwemo kurudisha maeneo ya hifadhi ili kurejesha uoto wa asili.