Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 4 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 63 2022-11-04

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. MOHAMED JUMAH SOUD aliuliza: -

Je, Kampeni ya AFR 100 imetekelezwa kwa kiasi gani na maendeleo gani yamefikiwa hadi sasa?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Jumah Soud, Mbunge wa Donge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara imefikia hatua zifuatazo katika utekelezaji wa Kampeni ya AFR 100: kuondoa wavamizi na kurejesha ardhi iliyoathiriwa; Kuimarisha usimamizi wa misitu ya mikoko; Kutoa elimu ya kudhibiti moto wa msituni ili kulinda uoto wa asili; na Kutekeleza Mpango wa Dodoma ya Kijani.

Mheshimiwa Spika, maendeleo yaliyofikiwa ni pamoja na kusainiwa kwa makubaliano ya Kurejesha Mandhari ya Kiafrika – (AFR 100) na Mbinu ya Tathmini ya Fursa ya Marejesho. Aidha, Tanzania imefanikiwa kuandaa na kukamilisha Mkakati wa Kitaifa wa Kurejesha Mandhari ya Misitu. Mkakati huu unatarajiwa kuwasilishwa katika Mkutano wa Nchi Wanachama wa kujadili masuala ya Mazingira (COP 27).