Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kitajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza naishukuru Serikali kwa barabara hii ya kuanzia Magole hadi Tuliani.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu jibu hili limekuwa la muda mrefu tangu 2010 mpaka sasa hivi mnaendelea hivyo hivyo, ndiyo jibu hilo hilo na kipande ni kilomita102 tu.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga bajeti kwenye kipande hiki cha Km 102 kwenye bajeti ijayo?

Swali langu la pili; je, barabara ya Lupilo mpaka Mahenge ni lini nayo itajengwa? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tumeshaanza kuijenga hii barabara hizo kilomita na hata katika bajeti ya mwaka kuna fedha imetengwa kwa ajili ya barabara hiyo, lakini Serikali inaendelea kutafuta fedha kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa iko kwenye mpango tunaweka katika miaka inayokuja ya bajeti tutaendelea kutenga fedha ili kuikamilisha barabara yote hii.

Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la pili kwa barabara ya Lupilo – Mahenge, barabara hii ni kati barabara kuu kwa maana ya trunk road na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wako Wakandarasi ambao tayari wameshapita Lupilo – Mahenge kwa ajili ya kuangalia kama itajengwa kwa mpango wa EPC. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii pia Serikali inategemea kuijenga kwa kiwango cha lami.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kitajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya kutoka Iringa kwenda Ruaha National Park, tayari ilishapewa fedha kwa maana zile fedha za mkopo.

Je, ni lini sasa Serikali itatangaza tender ili hiyo barabara ianze kujengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jackson Kiswaga, Mbunge wa Kalenga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ya kwenda Ruaha National Park Lusembe ina Kilomita 104 na inafadhiliwa na World Bank. Ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu zote za kuandaa zabuni zimeshakamilika na muda wowote itatangazwa kwa ajili ya kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami barabara yote. Ahsante.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kitajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Mkuyuni kupita Maina mpaka Mwatex yenye Km 11 tayari usanifu wake umekamilika.

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hiyo kwa lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K.
MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Furaha, Mbunge wa Viti Maalum – Mwanza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii ya Mkuyuni hadi Maina imeshafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, Wizara ya Ujenzi kwa kusaidiana na TAMISEMI tunatafuta fedha ili kuijenga barabara hii muhimu ambayo pia itakuwa kama bypass ya kuingia Mjini Mwanza. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu zinaendelea, kutafuta fedha kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kitajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Njiapanda - Rugali – Ndembe – Longa Km. 10, kwa mbele kuna lami lakini kipande hiki hakina lami. Je, ni lini Serikali itaunganisha kipande hiki kutoka Mbinga Mjini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Benaya Kapinga, Mbunge wa Mbinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoisema ni kweli ilijengwa mbele kwa sababu ya changamoto ya huko ilikojengwa ili kuhakikisha kwamba inapitika. Sasa hivi nimuhahakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatafuta fedha ili kukamilisha hiko kipande kilichobaki kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kitajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nilitaka kuuliza, kwa kuwa mchakato wa ujenzi wa barabara inayotoka Kakola kwenda Kahama umekalimika. Sasa ni lini na nini kimekwamisha Wizara kutangaza barabara hiyo ili ianze ujenzi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge tumekutana naye sisi na Wizara lakini pia na watendaji wa TANROADS. Ni barabara ambayo kweli fedha imeshapatikana, taratibu zinaandaliwa ili kuitangaza barabara hiyo. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hiyo mwaka huu wa fedha itaanza kujengwa.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kitajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara kutoka Babati-Galapo-Kimtoro hadi Kibaya?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Qwaray, Mbunge wa Viti Maalum Manyara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya kutoka Babati- Galapo kwenda Kibaya, tuanakamilisha usanifu wa kina; na mwaka huu itakamilika na baada ya hapo Serikali itaanza kutafuta fedha kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Kwa sasa usanifu wa kina unaendelea kukamilishwa. Ahsante.

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kitajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Barabara ya kutoka Mnivata-Tandahimba-Newala-Masasi kilometa 160 tunafahamu kwamba fedha zake zimepatikana na kipindi cha mvua karibia kinaanza.

Je, ni lini sasa ujenzi utaanza rasmi wa barabara hii kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maimuna Mtanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii inafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika, taratibu zote za zabuni na kuandaa zimeshakamilika. Kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu zote za manunuzi zitakavyokuwa zimekamilka, barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.