Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 4 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 55 2022-11-04

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: -

Je, ni lini kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kitajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara yote kutoka Magole - Turiani – Mziha hadi Handeni yenye urefu wa kilometa 147.7. Aidha, ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Magole – Turiani (Km 45.27) umekamilika na sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kukamilisha ujenzi wa sehemu iliyobaki ya Turiani - Mziha – Handeni yenye urefu wa kilometa 102.