Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza mchakato wa ujenzi wa Bandari ya Uvuvi katika Mji wa Kilwa Masoko?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kufuatia ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa Masoko, wananchi wa Kilwa Masoko tumeandaa eneo la kutosha kwa ajili ya sekta mbalimbali. Je, Serikali sasa iko tayari kuhakikisha kwamba sekta rafiki au taasisi rafiki na bandari ya uvuvi kama vile Chuo cha Uvuvi, viwanda vya kuchakata samaki pamoja na soko la samaki vinajengwa Kilwa Masoko?

Swali la pili, wapo wananchi wapiga kura wangu ambao wamefanyiwa tathmini ili kupisha ujenzi wa Bandari ya Uvuvi wakiwemo Ndugu Mwanawetu Zarafi, Ndugu Fatima Mjaka, Ndugu Fadhila Sudi pamoja na Ndugu Suleiman Bungara (Bwege) na wenzao 50.

Je, ni lini Serikali itakwenda kulipa fidia kwa wapiga kura wangu hawa. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa
Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza naomba nimhakikishie kuwa ujenzi wa bandari hii kubwa ya mfano na ya kielelezo katika Taifa letu inaendana na yote aliyoyasema ya uwepo wa miundombinu wezeshi. Kwa hivyo, nataka nikuhakikishie ya kwamba Serikali ya Awamu ya Sita imeliona jambo hili na nikipaumbele chake. Kutakuwepo na soko, patakuwepo na maghala ya kuhifadhia bidhaa za chakula, kutakuwepo na miundombinu mingine yote inayoendana na hadhi ya bandari ya uvuvi ya kisasa na ya Kimataifa.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, ni hili la tathmini naomba nilichukue jambo hili kwa kuwa jambo hili tunashirikiana na wenzetu wa Wizara ya Ujenzi kwa maana ya Mamlaka yetu ya Bandari (TPA), kwa hiyo nataka niwahakikishe nalichukua hili jambo nakwenda kulisimamia kuhakikisha kwamba wananchi hawa waweze kupata haki yao.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza mchakato wa ujenzi wa Bandari ya Uvuvi katika Mji wa Kilwa Masoko?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa ujenzi wa vizimba vya kufugia samaki katika Ziwa Duluti kwa lengo la kupunguza tatizo la ajira kwa vijana kule Arumeru Mashariki?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa
Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. John Pallangyo, Mbunge wa Arumeru, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita, inayoongozwa na Mheshimiwa Rais, Samia Suluhu Hassan ilitenga kiasi cha Shilingi Bilioni 20 kwa ajili ya kuanza mradi maalum wa vizimba vya Samaki. Vilevile tunao mradi kwa ajili ya maeneo ya ufugaji samaki nje ya vizimba kwa maana ya mabwawa. Naomba niseme tu kuwa Ziwa Duluti tutalifanyia tathmini ikiwa kama ni katika maeneo yenye kuweza kufanyiwa shughuli hizi za vizimba katika mwaka mwingine wa fedha tutaliwekea mpango na lenyewe, kwa sababu siyo kila mahali tunaweza kujenga vizimba kulingana na taarifa za kitaalam. Ahsante. (Makofi)