Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Forodha katika mpaka wa Olaika Wilayani Ngorongoro?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri, lakini nina uhakika kwamba tathmini ya mwisho kufanyika katika eneo hilo ni mwaka 2008.

Mheshimiwa Spika, basi naomba kumuomba Mheshimiwa Waziri kama inawezekana ili kuthibitisha yale anayoyasema tuongozane akaongee na wafanyabiashara wa Wilaya ya Ngorongoro ambao ndio wahitaji wa kituo cha forodha.

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa
Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Emmanuel Shangai, Mbunge wa Ngorongoro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote kabla ya kujibu swali hilo naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa namna anavyofuatilia na kufanyia kazi katika Jimbo lake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mama yetu Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungao wa Tanzania ni Serikali sikivu sana. Kwa hiyo, niko tayari kufuatana na yeye Mheshimiwa Mbunge kwenda katika eneo hilo na kuona uwezekano na kuongea na wananchi na wafanyabiashara kwa jumla. (Makofi)