Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 4 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 53 2022-11-04

Name

Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Forodha katika mpaka wa Olaika Wilayani Ngorongoro?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Lekishon Shangai, Mbunge wa Ngorongoro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, TRA ilifanya utafiti katika maeneo yote nchini yenye uhitaji wa Ofisi za kudumu za usimamizi wa kodi ikiwemo mpaka wa Olaika Wilayani Ngorongoro na kubaini kuwa gharama za usimamizi wa shughuli za forodha katika mpaka wa Olaika zitakuwa kubwa ikilinganishwa na kiwango cha ushuru wa forodha unaotarajiwa kukusanywa. Kwa muktadha huo, TRA itaendelea kufuatilia mwenendo wa ukuaji wa shughuli za forodha katika mpaka huo ili kufungua kituo cha forodha cha kudumu. Aidha, TRA itaendelea kuimarisha mfumo wa sasa wa kuhudumia mpaka huo ili kuwawezesha wananchi kuendesha shughuli zao za kibiashara kwa ufanisi zaidi.