Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya kutoka Igalukilo - Sayaka inayounganisha Mikoa ya Mwanza na Simiyu itahamishiwa TANROADS?

Supplementary Question 1

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa zoezi hili alilolisema Mheshimiwa Waziri hapo awali lilishawahi kufanyika na halikuwa na mafanikio na barabara hii ni muhimu sana kwa Mkoa wa Simiyu na Mkoa wa Mwanza. Je, nini maelekezo yake ya haraka kwa wafanyakazi wa TARURA ili zoezi lifanyike haraka ili tuweze kuunganisha barabara hii katika mikoa hii miwili?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Lusengekile, Mbunge wa Jimbo la Busega kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimeshatoa maelekezo kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Busega kupitia TARURA waanze mara moja mchakato huo ili nia ya Mheshimiwa Rais ya kupeleka huduma kwa wananchi na nia ya Mbunge wa jimbo lile kuhakikisha barabara hiyo inapitika muda wote ifikiwe.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, maelekezo haya nimeshayatoa na nayarudia tena na nitakuwa wa kwanza kuyafuatilia maelekezo hayo ili yaweze kutekelezeka.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya kutoka Igalukilo - Sayaka inayounganisha Mikoa ya Mwanza na Simiyu itahamishiwa TANROADS?

Supplementary Question 2

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona na kunipa nafasi. Tuna Barabara ya kutoka Makambako – Mlowa – Kifumbe ambako inakwenda kutokezea kule Ilunda. Barabara hii tumekuwa tukiiomba ipandishwe hadhi na kuwa ya TANROADS na kwa kuwa kule mbele inakotokezea barabara hii tayari ni ya TANROADS. Je, kwa nini sasa barabara hii inakoanzia isiwe ya TANROADS ikaunga na kule mbele ambako inatokea kwai le iliyo ndani ya TANRAODS?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge wa Jimbo la Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyotoa maelekezo katika swali la msingi la Mbunge wa Jimbo la Busega, niielekeze vilevile Halmashauri ya Makambako na Mkoa wa Njombe, kuhakikisha wanaanza na wao mchakato rasmi sasa ili barabara hii na yenyewe watu wa TANROADS, wakishapitisha vile vigezo vyao na wakaona inakidhi, iweze kupandishwa hadhi na kuwa barabara ya Mkoa ili iweze kusaidia wananchi wa eneo hilo.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya kutoka Igalukilo - Sayaka inayounganisha Mikoa ya Mwanza na Simiyu itahamishiwa TANROADS?

Supplementary Question 3

MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa
Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi barabara ya kutoka Bashineti – Lukumanda – Seche – Basodeshi – Ibadalu – Zinga, kutoka TARURA Kwenda TANROADS? Kwa sababu barabara hii upande wa Singida iko TANROADS na upande wa kutoka Babati kwenda Mbulu iko upande wa TANROADS.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hhayuma, Mbunge wa Hanang, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maelekezo yetu katika halmashauri zote nchini ikiwemo Halmashauri ya Hanang na mikoa yote, ni kuhakikisha zile barabara ambazo zinaunganisha kati ya halmashauri moja na nyingine, mkoa mmoja na mwingine ambazo zinaangukia katika upande wa TARURA ili ziunganishe mkoa, ni kuanza mchakato wa kuhakikisha sasa zinakuwa na vigezo vya kupandishwa hiyo hadhi.

Mheshimiwa Spika, maelekezo yangu kama katika swali la msingi na kwa Waheshimiwa Wabunge ni hayo na tutafuatilia maelekezo hayo kwa nia moja tu ya kutaka kuwasaidia wananchi katika maeneo yenu.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya kutoka Igalukilo - Sayaka inayounganisha Mikoa ya Mwanza na Simiyu itahamishiwa TANROADS?

Supplementary Question 4

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara inayotoka Mangaka Wilaya ya Nanyumbu - Nachingwea Tarafa ya Kilinalondo - Liwale katika Kata ya Ilombe, tumeshaiombea iingie TANROADS, lakini mpaka leo tunapigwa danadana.

Je, ni lini barabara hii itaweza kupandishwa hadhi kuwa barabara ya TANROADS kwa sababu barabara hiyo imepita katika wilaya tatu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Jimbo la Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ameshasema Mheshimiwa Mbunge walishaomba na mchakato upo katika ngazi husika na wenye jukumu la kufanya hivi ni watu wa TANROADS, naamini sisi Serikali ni moja tutalifuatilia ili kuharakisha huo mchakato uweze kukamilika. Ahsante sana.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya kutoka Igalukilo - Sayaka inayounganisha Mikoa ya Mwanza na Simiyu itahamishiwa TANROADS?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Je, ni lini Serikali itamalizia kipande kilichobakia kwenye Kawawa Road kufikisha Marangu Mtoni kwa hadhi ya lami, tulipewa ahadi na Mheshimiwa Rais Kikwete awamu zile na iko kwenye Ilani ya CCM?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Charles Kimei, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimwondoe hofu kwa sababu tumeshajenga awamu ya kwanza na kilichobaki nikumalizia katika eneo la pili na uzuri barabara hii iko katika mipango ya TARURA. Kwa hiyo, kwa sasa tunatafuta fedha tutakapopata mara moja naamini kabisa kwa sababu iko katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi barabara hii tutaitengeneza. Ahsante sana.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya kutoka Igalukilo - Sayaka inayounganisha Mikoa ya Mwanza na Simiyu itahamishiwa TANROADS?

Supplementary Question 6

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Mchakato wa kupeleka barabara za TARURA, kutoka TARURA kwenda TANROADS ni barabara ya kutoka Bukama – Mikulusanga – Mikomalilo tulishafanya mchakato na umekamilika. Sasa hoja ya kujiuliza ni kwamba TANROADS na TARURA wakitaka kupeleka barabara, vigezo vya kuwapelekea TANROADS wanasema sisi mpaka tupelekewe na Wizara. Sasa ni lini muunganiko huu wa TARURA na TANROADS utakuwepo ili barabara za TARURA ziondoke kwenye TARURA ziende TANROADS?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere, Mbunge wa Jimbo la Bunda Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba kuna muunganiko mzuri kati ya TANROADS na TARURA na tunafanya kazi kwa kushirikiana pamoja. Kwa hiyo, kinachofanyika tu ni kwamba kwenye zile barabara ambazo ziko chini yetu, huwa tunazipeleka kwao na wao wanaangalia vile vigezo vinavyostahili. Kwa hiyo, siyo kwamba wana nia ya kuchelewesha hizo barabara, ni kwa sababu wanaangalia vile vigezo, vikashakamilika wanatafuta fedha na ndiyo wanatangaza hizo barabara na kuwa za mkoa.

Mheshimiwa Spika, tutaendelea kuimarisha ushirikiano wetu ili haya maswali ya Waheshimiwa Wabunge tuweze kuyajibu kwa wakati na kwa urahisi zaidi. Ahsante sana.